ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, August 23, 2017

KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI SENGEREMA CHAVUNJIKA BAADA YA MGOMO.


KIKAO Cha baraza maalum la madiwani kilichokaa Tarehe 21/8/2017  katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema kimeahirishwa baada ya waheshimiwa madiwani kugoma kuendelea na kikao hicho, wakilalamikia kutopewa makabrasha kwa wakati kwa mujibu wa kanuni za vikao na kutokuwepo kwa CAG.
Wakiwasilisha hoja hiyo madiwani hao wamesema  kwa mujibu wa kanuni wanatakiwa kupata makabrasha hayo siku saba kabla ya kikao ili kuyapitia kifungu baada ya kifungu kwa umakini badala yake wameyapata jana hivyo hawajayapitika kwa kuyasoma na kuongeza kuwa mkuu wa wiliya alishaagiza wapatiwe makablasha hayo kwa kufuata utaratibu.

Akizungumzia sababu ya kucheleweshwa kwa makabrasha hayo mkurugenzi wa halmashauri ya Sengerema Bonifasi Mafuru Magesa amekili kosa hilo na kusema kuwa ni  kutokana na ratiba ya uzinduzi wa Mradi mkubwa wa maji ambao ulikuwa na ugeni wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Magufuli na Mwenge wa Uhuru ndiyo chanzo cha kutokupata makabrasha kwa wakati.BOFYA HAPA KUSIKIA KILICHOJIRI

Kwa upande wake mbunge wa Sengerema Mhe. William  Ngereja ameshauri kuahirishwa kwa kikao hicho kutoka na na mapungufu yaliojitokeza ili kukidhi vigezo.

Naye mkuu wa wilaya ya Sengerema Mhe. Emmanuel Kipole amesekitisha na ofisi ya mkurugenzi kwa kutokufuata utaratibu na maagizo ambayo aliyatoka katika balaza lililopita kwa kumtaka mkurugenzi kuhakikisha makablasha yanapatikana kwa wakati.

Akiahirisha kikao hicho mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya wa Sengerema ambaye pia ni diwani wa kata ya Nyamatongo  Mhe. Evarist Yanga ameunga mkono maamuzi ya waheshimiwa madiwani na kuahirisha kikao hicho hadi tarehe 23/8/2017

KIKAO HICHO KILICHOKUWA NA DHUMUNI LA KUPITIA NA KUJADILI TAARIFA ZA MKAGUZI WA HESABU ZA SERIKALI (CAG) KIMEAHIRISHWA HADI KESHO ALHAMISI YA TAREHE 24/8/2017 SAA TATU ASUBUHI.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.