Utafiti mpya umeonyesha kuwa asilimia 42 ya
wananchi wa Marekani wamepoteza imani na uongozi wa Rais Donald Trump wa
nchi hiyo katika kipindi cha siku 100 za kwanza ofisini.
Kwa mujibu wa utafiti huo uliofanywa na gazeti la Washington
Post-ABC News, kiwango hicho kimevunja rekodi kwa kuwa ni cha chini sana
na ambacho mara ya mwisho kilishuhudiwa nchini humo wakati wa utawala
wa Dwight Eisenhower, rais wa 34 wa Marekani aliyeongoza kati ya
mwaka 1953 na 1961.Asilimia 58 ya Wamarekani waliohojiwa wanasema Trump hana ufahamu kuhusu changamoto na masuala nyeti ambayo wananchi wa nchi hiyo wanataka kuona yakitekelezwa na utawala wake.
Hii ni katika hali ambayo, zaidi ya Wamarekani 40 elfu wakiwemo wasomi na wataalamu mashuhuri wa nchi hiyo wameshiriki kwenye maandamano mbele ya Ikulu ya Marekani White House, katika majengo ya Kongresi na Wizara ya Mazingira mjini Washington, kumpinga Rais Donald Trump wa nchi hiyo na kulalamikia sera zake za mazingira.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.