ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, April 12, 2017

JARIBIO LA MGOMO WA WALIMU NEEMA KWA 25

NA ANNASTAZIA MAGINGA, Mwanza

HALMASHAURI ya Jiji la Mwanza, imewalipa Walimu 25 waastafu stahiki zao Kabla ya   msululu wa kundi hilo kujazana kwenye ofisi za Mkurugenzi  Kiomoni Kibamba kufuatia maandamano yaliyokuwa yamepangwa  kupiga kambi wakidai malipo yao.

Akizungumza na waandishi  wa habari jana Mwenyekiti wa Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) Wilaya ya Nyamagana, Sibora Kisheri  amesema baada ya maazimio ya kikao chao na kuwasilisha taarifa kwa mwajiri wao na kuanza  kuchukuliwa  hatua  za haraka jambo ambalo limewafanya kusitisha mpango wa kuandamana na  kuweka kambi katika ofisi za mkurugenzi wa jiji hilo ili kulipwa stahiki zao.

Walimu hao   walikuwa wamejindaa kuweka  kambi isiyo na kikomo huku wakisisitiza kutoogopa kupigwa mabomu na polisi hadi watakapolipwa stahiki zao baada ya kufikia maamuzi yaliyoamuliwa hivi karibuni kwenye hafla ya kuwaaga Walimu 25 na kuwapatia zawadi ya  mabati 20 na Sh 20,000 kama nauli ambapo walilalamikia kitendo cha mwajiri wao kushindwa kuwalipa stahiki zao kwa muda muafaka jambo ambalo linaloendelea kuchochea maisha kuwa  magumu.

“Mpaka sasa walimu wastaafu 25, wameitwa na mkurugenzi na kulipwa nauli zao, pia walimu waliokuwa wamehamishwa vituo kati ya  mwaka 2016 hadi Machi mwaka huu wameanza kulipwa na taarifa nilizopewa  ni kwamba wamelipwa walimu 30 na zoezi linaendelea”amesema Kisheri.

Amesema  zoezi hilo linakwenda sambamba na walimu  waliokwenda likizo na kushindwa kulipwa ambapo deni lilifikia Sh milioni 205.75, na kwamba  wameanza kulipwa , huku  walimu wastaafu  Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF) wamekujasha chukua majina ya wastaafu ili kuingizwa katika malipo ya kila mwezi kulingana na asilimia ya mshahara wao.

“Kwa hatua zilizochukuliwa na mwajiri pamoja na PSPS wameona hakuna haja tena ya kuendelea na mpango waliokuwa wameazimia kwa lengo la kulipwa stahiki zao ambapo aliiomba Serikali kuacha  tabia ya kutotekeleza wajibu wao mpaka  shinikizo la watumishi”amesema Kisheri.
 Amesema  imekuwa mazoea kwa serikali kutekeleza madai ya walimu pale wanapotangaza mgogoro  huku akihoji wapi fedha zilipotoka na kuanza kuwalipa  wakati awali Mkurugenzi wa jiji hilo, Kibamba alidai hana fedha.

Akizungumza kwa niaba ya walimu wenzake wastaafu, Eliamin Msangi, ameeleza  hivi sasa waastafu wamekuwa wakiona jambo la  kustaafu ni kama janga kwao kutokana na kile waajiri wao hushindwa kutekeleza licha ya   kuwa hatua hiyo ni muhimu  kwani kipindi hicho ni cha kupumzika na kubaki mshauri kwa wafanyakazi waliobaki kwenye utumishi.

“Unapostaafu tu mshahara unakoma mara moja, leo tunapozungumza hapa baadhi yetu tumekuwa kero kwenye nyumba za walimu tunaambiwa tuondoke ili mwalimu mwingine aingie, sisi wastaafu wa mwaka jana tumeathiriwa sana na zoezi la uhakiki wa  vyeti na  watumishi hewa kwani hesabu zetu zimepigwa kwa madaraja ya chini” amesema Msangi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.