ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, March 30, 2017

KAMBI YA UPINZANI CONGO YAWATAKA WANANCHI KUNZISHA OPERESHENI "MJI WA MAZIMWI"


KAMBI ya upinzani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imewataka wananchi wa nchi hiyo kuketi majumbani mwao Jumatatu ijayo na kutotoka nje ili kumlazimisha Rais Joseph Kabila wa nchi hiyo kutekeleza makubaliano ya kugawana madaraka. 
Taarifa iliyotolewa na muungano wa kambi ya upinzani imesema kambi hiyo itaanzisha operesheni ya "mji wa mazimwi" kwa ajili ya kusimamisha shughuli zote kote nchini Congo.

Muungano huo  umesema machafuko ya sasa nchini humo yamesababishwa na hatua ya Rais Joseph Kabila ya kukataa kutekeleza makubaliano ya kugawana madaraka yaliyotiwa saini Disemba 31 mwaka jana.

Makubaliano hayo ambayo yalisimamiwa na maaskofu wa Kanisa Katoliki, yalimruhusu Rais Kabila kubakia madarakani baada ya kumalizika muhula wake wa uongozi hadi mwishoni mwa mwaka huu sambamba na kuunda serikali ya mseto itakayoongozwa na Waziri Mkuu atakayetoka kambi ya upinzani.
Rais Joseph Kabila wa Congo

Makumi ya raia wameuawa katika machafuko na maandamano ya raia wa Congo DR wanaomtaka Rais wa nchi hiyo Joseph Kabila ang'atuke madarakani.  

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.