ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, November 18, 2016

MAMA SAMIA AMALIZA ZIARA YAKE MKOANI MWANZA.










Halmashauri zimetakiwa kuacha kuilalamikia  serikali kila mara kuhusu ufinyu wa bajeti na badala yake ziongeze bidii ktk ukusanyaji wa mapato, kuzuia upotevu wake na kubuni vyanzo vipya vya mapato.

Akizungumza na viongozi na watendaji mbali mbali wa chama na serikali katika majumuisho ya ziara yake ya siku nne mkoani Mwz Makamu wa Rais Mama SAMIA SULUHU HASSAN ameutaka mkoa wa Mwz kuhakikisha inamaliza tatizo la uhaba wa madawati.

Makam wa rais Mama SAMIA SULUHU HASSAN amehitimisha ziara yake mkoani Mwz kwa kutembelea machinjio ya jiji la MWZ ambayo yako katika ukarabati Mkubwa na kuweka jiwe la msingi kabla ya kutembelea na kuzindua Makao Makuu ya Halmashauri ya wilaya ya Ilemela
Akihubia mamia ya wakaazi  wa Mandu nyakato jijini MWZ SAMIA ameitaka halmashauri ya jiji kutumia teknolojia ya kisasa huku akihadharisha  halmashauri ya jiji kuhusu usimamizi wa mradi huo.

Awali akiwasilisha taarifa ya maendeleo ya halmashauuri hiyo Mkurugenzi wa Halmashari ya jiji la Mwz KIOMONI KIBAMBA aliitaka serikali kusaidia ununuzi wa vifaa vya kisasa.

Akifanya majumuisho ya ziara yake mkoani Mwz Makamu wa Rais Mama SAMIA SULUHU HASSAN amemtaka mkuu mkoa wa Mwz JOHN MONGELA kuhakikisha anamaliza tatizo la uhaba wa madawati ifikapo Januari mosi 2017.

Makamu wa rais Mama Samia Suluhu Hassan amehitimisha ziara yake ya siku nne  mkoani Mwz ambapo amekagua, amezindua na kuweka jiwe la msingi katika mabweni ya wasichana, kituo cha afya, mradi wa maji , machinjio ya kisasa, na kuhutubia mikutano ya hadhara.

ZEPHANIA MANDIA WA G.SENGOBLOG.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.