ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, November 30, 2016

HOJA YA SIMBA NA YANGA KUTUMIA MAREFA WA NJE YA NCHI NI UPUUZI

Baada ya kauli ya Viongozi wa klabu ya Simba kusema kuwa hautacheza mchezo wowote wa ligi dhidi ya watani wao wa jadi Yanga endapo waamuzi hawatatoka nje ya nchi tena wenye uzoefu wa mechi kubwa wanaotambuliwa na FIFA. 

Wachambuzi wa Soka toka kituo cha Redio Jembe Fm ya jijini Mwanza wamelipambanua suala hilo na kulichimba kwa undani kisha kuja na majibu kuwa hoja hiyo haitekelezeki, na ni hoja ya kuliondoa soka la Tanzania kwenye ramani ya soka Ulimwenguni.

Simba wametamka bayana kuwa wapo tayari kulipa gharama za waamuzi hao kuanzia mwamuzi wa kati na wasaidizi wake wawili ili haki itendeke kwakua watani wao wamekuwa wakipendelewa mara kwa mara na marefarii wa hapa nchini. 

Msimamo huo umetolewa na msemaji wa klabu hiyo Haji Manara alipokuwa akizungumza na waandishi wa Habari klabuni hapo na kusema kuwa kwasasa hawatakuwa tayari kuona haki zao zikidhulumiwa kwa namna yoyote na wataanzia mzunguko wa pili unaotarajia kuanza Disemba 17.

Fuatilia kilichojiri ndani ya uchanbuzi katika kipindi cha KIPENGA kinachoruka kila jumamosi saa 07:00 asubuhi hadi 10:00 asubuhi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment