ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, September 26, 2016

WATANZANIA WATAMBA ROCK CITY MARATHON 2016.

 WATANZANIA watamba na kurudisha heshima ya nchi baada ya kuibuka kidedea wa mashindano ya  mbio za Rock City Marathon yalioandaliwa na Capital Plus International Ltd yaliyodhaminiwa na mfuko wa pesheni wa (NSSF) huku yakisapotiwa na Jembe FM kama wadau wa masuala ya uhamasishaji.

Mbio zilizokuwa gumzo zaidi ni zile za kilomita 21 ambapo washiriki toka  nchi za Afrika Mashariki na kati, Kenya, Uganda, Rwanda, Zambia, Burundi na wenyeji Tanzania walijitokeza na kushiriki.

Michuanao hiyo ilikuwa imegawanyika katika makundi mbalimbali ya Km 21,5,3 na 2 ambapo washindi wote wa kwanza upande wa wanaume na wanawake ni washiriki kutoka Tanzania upande wa  Km 21 ni  Chacha Boy na Thailun Abdul wakijinyakulia sh milioni moja na nusu kwa kila moja ikiwa na medali na Cheti.

Aidha kwa upande wa kilomita  5  kwa wanawake na wanaume walijinyakulia zawadi ya sh laki tisa na medali na Cheti ni Barnad Samike naHelena Bahati na Km 3, Germia Kinshuli na Chirstina Urio na Km 2 ni Winefrida Mathayo naSamsoni paul. 

Naye meneja wa NSSF Hamisi Fakii amesema ili Tanzania ipate mafanikio katika sekta ya mchezo wa riadha wananchi wanapaswa kujitokeza kwa wingi kushiriki michuano hiyo na kuipa msisimko nalo shirika lake likiahidi kujitokeza kila mwaka kudhamini mashindano hayo ili kuhakikisha kukuwa kwa michezo nchini ikiwa ni moja wapo ya ajira kwa vijana na wazee.

GSENGO BLOG ikizungumza na washindi hao walisema wanamshukuru mwenyezi mungu kwa kuibuka washindi na kuipeperusha vyema Tanzania kwani miaka ya nyuma washiriki wa nchi zingine ndio walikuwa wanajinyakulia ushindi hivyo jitihada zao na mazoezi ndivyo vilivyowafanya kuwa washindi.

Walisema maandalizi ya mwaka huu yalikuwa mazuri japo kuwa walikabiliwa  na changamoto ya magari kwa sababu mpangilio  haukuwa mzuri walipokuwa wakimbia wanapishana na magari kitu ambacho ni hatari kwa maisha yao pia waliwataka watanzania kufanya mazoezi kwani ni msingi mzuri kwa maisha yao  utakao saidia kupeperusha Bendera ya Taifa na kuwafanya nchi zingine waone Tanzania
inaweza  kuliko wao.

Naye mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongella ambaye alikuwa mmoja wa washiriki  aliwashukuru wadhamini walioandaa mashindano hayo NSSF, NMB, Mwanza hotel, FABEC, Real Pr Solution, Puma Energy, TIPER na Friekdin Conservation Fund kwa kuona umuhimu na kujali thamani ya michezo pia aliwataka waendelee kujitoa na kudhamini na vitu vingine ili kuleta maendeleo zaidi.






























Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.