ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, September 4, 2015

MWANAFUNZI WILAYANI KISARAWE MKOA WA PWA AMTOROKA MUMEO BAADA YA KUOZESHWA NA BABA YAKE KWA NG'OMBE 150

VICTOR MASANGU, PWANI UKATILI KWA WATOTO
WAZAZI na walezi hapa nchini wametakiwa kuachana na mila zilizopitwa na wakati kwa kuwaozesha watoto wao mapema hususan wa kike  wakiwa katika umri mdogo na kupelekea baadhi yao kukatisha masomo yao na badala yake wawe na mawazo chanya ya kuwasaidia katika kuwalinda na kuwapatia haki zao za msingi katika elimu.

Kauli hiyo imetolewa na mwanafunzi mmoja anayesoma kwa sasa kidato cha tatu  ambaye jina lake linahifadhiwa kutokana na kulinda haki za watoto wakati wa ziara ya siku mbili Wilayani Kisarawe Mkoa wa Pwani  iliyofanywa na shirikika la kimaendeleo linalojishughulisha na kutoa misaada kwa binadamu Plan International kwa lengo la kubaini changamoto  zinazowakabili watoto.

Mwanafunzi huyo akizungumza kwa majonzi  na waandishi wa habari pamoja na watendaji wa halmashauri ya Kisarawe pamoja na watumishi wa Plan international  amesema kwamba amesikiteshwa sana kuona wazazi wake wanamkatisha masomo yake na kumwozesha kwa nguvu bila lidhaa yake kwa mwanaume.

Aidha binti huyo amebainisha kuwa baada ya mwaka 2014 mwanzoni  kumkatalia baba yake mzazi kuolewa ndipo mazi wake alipoamua kutumia njia nyingine ya kumdang’anya anamtafutia uhamisho wa kwenda kusomea shule nyingine iliyopo Wilayani Mkuranga kumbe  alikuwa tayari amemtafutia mwanaume  kwa nguvu kwa lengo la kumwozesha mwanae wa kumzaa.

Kwa upande wake Afisa ustawi wa Jamii Wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani amethibitisha kutokea kwa taarifa za tukio hilo la mwanafunzi na kwamba wamempokea na kumpatia msaada wa hali na mali ikiwemo kumpatia mahitaji muhimu na kumpeleka shule ambapo kwa sas  anaendelea na masomo.

Kwa upande wake mmoja wa mjumbe wa kamati ya ulinzi ya mtoto Wilaya ya Kisarawe Saimon Mpunga akizungumza kwa niaba ya wajumbe wenzake amesema kwamba kuja haja ya kuwafichua wazazi wenye tabia kama hizo na kuongeza kuwa baada ya mradi huo wa wa kupinga ukatili dhidi ya watoto kuanziashwa na Plan International jamii imeweza kuvunja ukimya.
  
Jembe Fm iliweza kupata fursa ya kuzungumza na mama mlezi  ambaye anamlea mwanafuzni huyo kwa sasa aliyejitambulisha kwa jina la Veronica Kilango na hapa alikuwa na haya ya kusema kuhusiana na msicha huyo.

Kuanzishwa kwa Mradi   huo wa Plan International  wa  kupinga ukatili dhidi ya watoto umeweza kusaidia kwa kiasi kikubwa  na kufanikiwa kumpata na kumsaidia  mwanafunzi huyo ambaye aliozeshwa  na baba yake mzazi   kwa mwanaume mwenye umri wa mika (30) kwa ng’ombe 150.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.