ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, January 6, 2015

SAFARI LAGER WEZESHWA

Meneja wa Bia ya Safari Lager, Edith Bebwa(kushoto) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani ) wakati  kutangaza upatikanaji wa fomu za kuomba ruzuku za wajasiliama kwa msimu wan ne wa program ya Safari Lager Wezeshwa  uliofanyika Dar es Salaam jana.Kulia ni Jaji wa Programu hiyo, Joseph Migunda.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Toleo la Leo

SAFARI LAGER YATANGAZA RASMI UPATIKANAJI WA FOMU ZA PROGAMU YA SAFARI LAGER WEZESHWA MSIMU IV.
Dar es Salaam, Jumanne  Januari 6, 2015: Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya Safari Lager leo imetangaza rasmi upatikanaji wa fomu za programu yake ya Safari  Lager Wezeshwa kwa msimu wa nne kwa wajasiriamali wadogo wadogo  na wa kati  Nchini.  

Akizungumza  na waandishi wa habari, Meneja wa bia ya Safari Lager Bi. Edith Bebwa  alifafanuwa ya kwamba “ Fomu za ushiriki zitapatikana kwenye mabohari ya TBL, Mawakali wa kusambaza bia, kwenye mtandao wa www.wezeshwa.co.tz . Fomu hizo zichukuliwe, zijazwe na kurejeshwa kwenye vituo vilivyotajwa hapo juu au kwa njia ya posta kwa sanduku la posta (Safari Lager Wezeshwa msimu wa nne,Tbl Dar es Salaam,P.o Box 9393 DSM).
Alisema Bi Edith, hii ni hazina tosha kwa wajasiriamali wadogowadogo nchini kwani itarahisisha kazi  kwa kuwepo na vitendea kazi bila ya kutumia nguvu nyingi”.
Programu hii ni msimu wa nne   tangu kuanzishwa kwake na  imeleta mafanikio makubwa kwa wajasiriamali waliopata uthubutu wa kujaribu kujiunga na hatimae kuongeza uchumi wa nchi.

Programu hii itafanyika takribani mikoa yote ambapo itawapa fursa wajasiriamali wa aina zote bila kujali fani,kabila wala jinsia  kujaza fomu kwa usahihi na kamilifu   kisha kuzirudisha mahala husika na baadae waliokidhi nafasi zinazohitajika kuchaguliwa kisha kupewa mafunzo mafupi  pamoja na kukabidhiwa ruzuku  zao alisema Bi Edith.

Meneja wa bia ya Safari Lager, Edith Bebwa alimaliza kwa kutaja tarehe ya mwisho wa kurejesha fomu kuwa ni 20,Februari 2015 hivyo wajasiliamali wanapochukua fomu wakumbuke pia muda wa kuzirejesha walipozitoa.

Nae kiongozi wa wataalamu wa ushauri wa biashara kutoka kampuni ya TAPBDS, Bwana Joseph Migunda alisema kuwa  “Zoezi hili linahusisha wataalamu wenye uwezo na uzoefu mkubwa katika kushauri na kusaidia ukuzaji wa sekta ya biashara ndogo na kubwa. Hivyo aliomba wajasiriamali wote kuitumia fursa hii kushiriki kwa kuzingatia vigezo vilivyoainishwa kwenye fomu ya ushiriki. Wenye nia ya kufika mbali kibiashara na wenye  malengo ya kuisaidia jamii inayowazunguka wasisite kuchangamkia fursa hii”.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.