ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, July 29, 2014

LIGI YA EPL VERY SOON KUANZA KUTIMUA VUMBI, USAJILI NAO UMECHACHAMAA.

Cedrick A. G. Sengo (L) na Cuthbert A. G. Sengo (R)
Divorc Origi katika mojawapo ya mechi za Ubelgiji
Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Ubelgiji Divorc Origi hatimaye amejiunga na timu ya Liverpool.

Baba yake Origi, Mike Okoth, ambaye ni mchezaji wa zamani wa timu taifa ya Kenya Harambee Stars amethibitsha mwanawe Divorc amesaini mkataba na Liverpool ambao walifurahishwa na mchezo wake mzuri alipoiwakilisha Ubelgiji kwenye kombe la dunia.
Arsenal yamsajili Chambers
Kilabu ya Uingereza ya Arsenal imemsajili mlinzi wa kilabu ya Southampton Calum Chambers kwa takriban paundi millioni 16.
Mchezaji huyo wa timu ya Uingereza isiozidi umri wa miaka 19 alifanyiwa ukaguzi wa kimatibabu siku ya ijumaa.
Chambers mwenye umri wa miaka 19 ameshiriki mara 25 katika timu ya soka ya taifa la Uingereza na kwamba Arsenal inamuona kama suluhu wa safu ya ulinzi wa kulia na katikati .
Arsenal pia inamsaka mchezaji wa kiungo cha kati wa Southampton Morgan Schneiderlin mwenye umri wa miaka 24 ambaye aliichezea timu ya Ufaransa katika kombe la dunia.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.