ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, May 4, 2014

WAANDISHI WAASWA KUSIMAMIA KWELI.

Mgeni  rasmi   Jaji  Warioba  akiwahutubia  maadhimisho  ya  uhuru wa vyombo  vya  habari  kwenye  ukumbi wa mbayuwayu (AICC)
Mta  mada   juu ya  ushuhuda  Edwin Soko akiwasilisha  mada  katika maadhimisho  hayo.
WAANDISHI  Nchini wametakiwa  kutokata  tamaa  katafuta  na kuripoti  habari zao  zenye  ukweli  kwa jamii  ili  kuchochoea  maendeleo  bila  kuogopa  vikwazo  mbalimbali   toka  kwa  dola  ya  Nchi.
 
Hayo  yamesemwa   leo  na  jaji mstaafu  Mark  Boman  kwenye  kilele  cha  maadhimisho ya  uhuru  wa vyombo vya  habari  duniani yaliyofanyika  jijini  Arusha  kwa kuwakutanisha  zaidi ya waandishi wa  habari 500.
 
Jaji  Boman  alisema  kwa  sasa  waandishi  lazima waongeze  juhudi  katika  kazi  zao  bila  kuogopa   kutishwa  au kusongwasongwa  na  watawala  au  kundi fulani  la  watu  wenye  kutaka  maslahi  yao  yalindwe  na  kuwaumiza  wengine  walio wengi.
 
Aliongeza kuwa  mwandishi  lazima  awe na  uwezo wa kupata  taarifa na kuzifanyia  uchambuzi na kuzifikisha  kwa  jamii  kwa muda  mfupi  na kuisaidia  jamii  kwa ujumla.
 
Maadhimisho  hayo yalitanguliwa  na uwasilishaji wa mada  toka  kwa wataalamu mbalimbali , zilizotoa  mifano ya  kuminywa  kwa  uhuru  wa vyombo  vya  habari  Tanzania.
 
Pia  baadhi ya waandishi walitoa ushuhuda   kwa  matatizo mbalimbali  yaliyowapata  wakati wakitekeleza kazi  zao. 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.