ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, April 4, 2014

WAONYESHA UZALENDO KWA KUSAFISHA MIFEREJI MTAA MZIMA.

Ili kuonyesha kuwa wamehamasika na kampeni ya Onyesha Uzalendo Tangaza Upendo iliyoasisiwa na kituo Cha Radio Clouds Fm nchini, vijana wa mtaa wa Mwaloni karibu na soko kuu la samaki Mwaloni Kirumba Mwanza wameamua kujitolea kuzibua mifereji ya maji taka mtaa mzima ili kurahisisha utiririshaji wa maji kipindi cha mvua.
Vijana hao wapatao saba ambao walisema majina yao siyo muhimu zaidi ya vitendo wamesema kuwa ni elimu tu inahitajika kwa jamii yetu kubadilika na kuwa watekelezaji zaidi ya wazungumzaji na kwa kuliona hilo wameamua kuanza katika mtaa wao ili vijana wegine waige mfano.

Wamesema kuwa utunzaji wa mazingira ni njia ya kuendeleza afya kwa njia ya kuzuia mawasiliano ya binadamu na athari za taka. Athari zinaweza kuwa za kimwili, mikrobiyolojia, biyolojia au kemikali vikolezo vya ugonjwa. 

Wameyafanya hayo wakijua kabisa kuna baadhi ya wananchi wenzaomtaani hutupa taka zisizo pashwa kutupwa kwenye mifereji ya wazi kama  vile kinyesi, taka ambazo zinaweza kusababisha matatizo ya afya kwa binadamu na wanyama.

  Taka nyingine zisizofaa kwa mifereji ya mitaani iliyo wazi ni pamoja na taka ngumu, maji machafu, taka za viwandani, na taka za kilimo. 

Usafi kama huu ni njia ya kuzuia magonjwa unaweza kutumika kwa ufumbuzi handisi (kama majitaka na matibabu ya maji machafu.

Upungufu wa usafi wa mazingira ni sababu kuu ya maradhi duniani kote hivyo uboreshaji wa mazingira una manufaa makubwa kujikinga na athari mbalimbali kwa afya ya wote katika kaya na katika jamii. Big up kwa kuonyesha Uzalendo kwa vijana wa Kirumba.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.