ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, October 16, 2013

UZINDUZI MBIO ZA MITUMBWI KANDA YA ZIWA 2013

Meneja Masoko wa Kampuni ya Bia Tanzania(TBL), Fimbo Butallah(kushoto) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa mashindano ya Mitumbwi kwa kanda ya Ziwa yanayodhaminiwa na Bia ya Balimi Extra Lager.Uzinduzi huo umefanyika Dar es Salaam leo.Kulia ni Mratibu wa mashindano hayo, Peter Zacharia. Picha kwa hisani ya Integrateg Comminication Limited.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Toleo la Leo
 
BALIMI EXTRA LAGER YATANGAZA RASMI UDHAMINI WA MASHINDANO YA MBIO ZA MITUMBWI KANDA YA ZIWA KWA MWAKA 2013.
 
Dar es Salaam, Jumatano 16 October 2013: Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya Balimi Extra leo imetangaza rasmi kudhamini kwa mara nyingine tena mashindano ya mbio za mitumbwi kwa wakazi wa kanda ya ziwa kwa mwaka huu 2013. Mashindano haya ya “kupiga makasia” yanafanyika kwa mwaka wa kumi na nne mwaka huu na yamekuwa na hamasa na msisimko mkubwa kwa wakazi wa maeneo hayo.
 
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar Es Salaam leo, Meneja Masoko wa kampuni ya Bia Tanzania (TBL) Bwana Fimbo Butallah alisema kwamba lengo hasa la Bia ya Balimi Extra kudhamini mashindano haya ni kufurahi pamoja na wakazi wa kanda ya ziwa hususani wale ambao ni wavuvi. Aliendelea kusema, “Mashindano haya yanaenzi na kulinda tamaduni zetu zisipotee, yanajumuisha watu mbalimbali kukutana, kufahamiana na kufurahi kwa pamoja na hii inasaidia sana kuimarisha amani na upendo baina yetu. Amani ni nguzo muhimu sana kwa Taifa letu”. Alisisitiza pia umuhimu wa michezo katika kujenga afya bora.
 
Bwana Fimbo alifafanua kwamba kwa mwaka huu mashindano ya mitumbwi yatahusisha miji mitano ya kanda ya ziwa. Yataanza rasmi mchakato wake Jumamosi hii tarehe 19 October katika mji wa Kigoma na kisha kuelekea mji wa Bukoba katika mkoa wa Kagera. Yataendelea mjini Mwanza, kisha katika kisiwa cha Ukerewe ambapo yatamalizikia katika mji wa Musoma. Washindi watakaopatikana katika miji hii watashindanishwa kwa pamoja ili kumpata mshindi wa kanda. Shindano la kumpata mshindi wa kanda linategemewa kufanyika jijini Mwanza mwanzoni mwa mwezi December. Tarehe za mashindano haya ni kama ifuatavyo;
 
1.    Mji wa Kigoma; Jumamosi tarehe 19 October               Ufukwe wa Kibirizi.
2.    Mji wa Bukoba; Jumamosi tarehe 02 November           Ufukwe wa Spice Beach.
3.    Mji wa Mwanza; Jumamosi tarehe 09 November          Ufukwe wa Mwaloni.
4.    Kisiwa cha Ukerewe; Jumamosi 16 November                        Ufukwe Hoteli ya Monarch.
5.    Mji wa Musoma; Jumamosi tarehe 23 November         Ufukwe wa Bwalo la Polisi.
6.    Mashindano ya Kanda; Jumamosi tarehe 07 Dec        Ufukwe Mwaloni, Mwanza.
Bwana Fimbo akizungumzia zawadi za mwaka huu alisema kwamba katika ngazi ya mikoa na ngazi ya kanda Balimi Extra imetenga zaidi ya shilingi milioni ishirini na nne kama zawadi za pesa taslimu kwa washindi. Mpangilio wa zawadi ni kama inavyoonekana hapa chini;
 
ZAWADI
NGAZI YA MKOA
WANAUME
NGAZI YA MKOA
WANAWAKE
NGAZI YA KANDA
WANAUME
NGAZI YA KANDA
WANAWAKE
Mshindi wa Kwanza
900,000
700,000
2,700,000
2,300,000
Mshindi wa Pili
700,000
600,000
2,300,000
1,700,000
Mshindi wa Tatu
500,000
400,000
1,700,000
900,000
Mshindi wa Nne
400,000
300,000
900,000
700,000
Mshindi wa 5 - 10
6 @ 250,000
6 @ 200,000
6 @ 400,000
6 @ 250,000
 
 
Bwana Fimbo alimaliza kwa kuwaomba wanachi wa kanda ya ziwa wajitokeze kwa wingi katika miji iliyotajwa ili kufurahi kwa pamoja katika matamasha haya. Alisisitiza wasisahau mila na tamaduni zao katika kipindi ambacho watu wengi hupenda kuiga tamaduni za kimagharibi. Alimaliza kwa kuwashukuru sana wanywaji wa bia ya Balimi Extra kwa kuchagua bia hii na kuomba waendelee kuitumia kwani ni kupitia mchango wao ndipo pia Balimi Extra Lager inaweza kuleta burudani kama hizi kwa ajili yao.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.