ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, October 26, 2013

BAADA YA MASHABIKI WAKE WATANO KUFA KWENYE AJALI: RUSUMO FC YAFANYA TAMASHA LA KUMBUKUMBU

 Bango la Kumbukumbu
Makamu M-Kiti NDFA akikabidhi Rambirambi 200,000 kwa Mwenyekiti wa Klabu
Wanafunzi wakiimba wimbo maalum Kuwakumbuka marehemu hao.
Utulivu kwa Dua ya Kuwakumbuka
Kulia ni Shabiki wa Rusumo Fc (Emma), Suley Mohamed Mfadhili wa Rusumo Fc, Upupu na Brayan.
Kushoto Makam M-Kiti Chama cha soka wilaya Ngara (NDFA) Seif Upupu, Brayan na OCD
RUSUMO FC
RUSUMO VETERAN
OCD Abel Mtagwa (Kulia) Godfrey Byaran na Mwisho Kabisa Makam M-Kiti chama cha soka wilaya Seif UpupuMTAGWA NA BRAYAN
Wa pili kulia ni OCD Ngara na Viongozi wengine.
Tamasha limefanyika mwishoni mwa wiki iliyopita katika Uwanja wa Shule ya Msingi Nyakahanga, kijiji cha Rusumo Mpakani mwa Tanzania na Rwanda upande wa wilaya ya Ngara mkoani Kagera

Mgeni Rasmi alikuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi wilaya(OCD) Abel Mtagwa, Mgeni wa Heshima Makamu mwenyekiti wa Chama cha Soka wilaya ya Ngara (NDFA) Seif Omary Upupu aliyeambatana na Mwakilishi wa Vilabu Godfrey Brayan

NDFA kilitoa rambirambi ya Sh Laki mbili (200,000) kwa klabu kisha kufanyika harambee ndogo kwa ajili ya kuwapa wafiwa na ilipatikana Sh laki mbili na Thelathini (230,000)

Tamasha hilo lilianza kwa maandamano kutoka kituo cha Forodha Rusumo hadi Uwanjani na kisha kumalizika kwa mchezo wa mpira wa miguu kati ya Rusumo Fc na Rusumo Veterans ambapo Maveterani walifungwa magoli 4-1

Klabu ya Rusumo Fc ilipata mkasa wa kuondokewa na mashabiki wake watano Tar 14.10.2012 baada ya kupata ajali majira ya saa mbili usiku katika eneo maarufu kwa jina la Zerozero nje kidogo ya mji wa Ngara wakati wakitokea Kabanga kucheza mechi ya Nusu Fainali ya michuano ya kombe la Polisi jamii wakiwa na gari la jeshi la polisi ambalo liligonga jiwe na kupinduka katika eneo hilo ilipo njiapanda ya barabara ya kwenda Rwanda kupitia Rusumo na ile ya Burundi kupitia Kabanga ambapo watu watano walifariki dunia.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.