Emanuel Mgaya aka Masanja Mkandamizaji akizungumza na kusanyiko lililojitokeza kwenye mazishi ya Askofu wa EAGT hayati Moses Kulola aliyefariki na kuzikwa kwenye eneo la wiwanja vya kanisa la EAGT Bugando jijini Mwanza.
Mbali ya kuwa mchekeshaji mahiri, Masanja Mkandamizaji ana karama ya uinjilisti, akitambulika kama Mchungaji wa kanisa la Mito ya Baraka. Katika mazishi ya Askofu kulola, Masanja alipata nafasi ya kuimba (kwani ana album ya muziki wa Injili) katika ufafanuzi wa moja ya nyimbo zake alisema "Hakuna mstari kwenye Biblia usemao 'baada ya kifo ni kesi', bali kuna unaosema 'baada ya kifo ni hukumu'," Kisha akaongeza... "Kuna tofauti kati ya kesi na hukumu, kesi unasomewa na kujitetea na mengineyo ya kutafuta ushahidi, lakini hukumu ni kwamba mambo yoooote yamejulikana na sasa kinachobakia ni kusalimika ukarejea uraiani au kukutana na kifungo"
"Ingekuwa baada ya kifo ni kesi hakuna Mtanzania angeenda motoni kwani Watanzania ni mafundi kwenye kujitetea hivyo Mungu aliliona hilo....."(Bofya play kumsikiliza.)
KATIKA PICHA MAPOKEZI YA MWILI WA BALOZI DR KAMALA
-
Ni Simanzi kubwa mapokezi ya Mwili wa Balozi Kamala
Jeneza lenye Mwili wa mpendwa wetu
Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Mh Erasto Siima amewaongoza wananchi katika...
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.