ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, September 13, 2013

AUNGUZWA VIDOLE NA MAMA YAKE MKUBWA KISA KUDOKOA MBOGA.


Blogger G. Sengo akiwa amembeba mtoto Winfrida Nicolaus aliyeunguzwa na mke wa baba yake mkubwa ambaye ni askari polisi, kwa madai ya kudokoa mboga.
ALBERT G. SENGO.
MTOTO Winfrida Nicolaus ( miaka zaidi ya 8)ameunguzwa vibaya na moto  kwenye vidole vyake vya Mkono wa kulia kwa kutuhumiwa kudokoa minofu miwili ya nyama kwenye sufuria na mke wa Baba yake mkubwa ambaye ni Askari polisi Mkoani hapa maeneo ya Nyansaka Wilayani Ilemela Jijini Mwanza.

Akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea katika Kituo cha Kuzuia na Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Watoto Majumbani kilichopo eneo la Kiloleli Wilayani hapa alipohifadhiwa na kupatiwa matibabu, alisema kwamba mama yake huyo alimkamata na kumfunga kitambaa mkono wa kulia kisha kummwagia mafuta ya taa na kuwasha kiberiti na kumchoma moto.

Kitendo hiki ni cha kinyama kisichokubalika kwa jamii kutokana na hatua zilizochukuliwa na Mke wa Askari Polisi huyo cha kumfuata mtoto Winfrida kijijini kwao na  kumchukua kuja kuishi naye kwa lengo la kumlea kumbe akija kumfanyia ukatili na kumsababishia ulemavu wa mkono wake wa kulia ambao vidole vyote vitano alivichoma moto kwa mafuta ya taa.

“ Alinishika na kusema eti nimedokoa nyama minofu miwili niliposema sio mimi alinichapa fimbo kila sehemu na akanifunga kitamba na kunimwagia mafuta ya taa na kunichoma na moto wa kiberiti nililia lakini alikuwa nananifungia ndani ili watu wasinione” alisimulia mtoto huyo

Afisa Ustawi wa Jamii kituo cha Foundation Karibu Tanzania Johanes Emmanuel (kulia).
Naye Afisa Ustawi wa Jamiii Kituo cha Foundation Karibu Tanzania Johanes Emmanuel alisema kuwa kutokana na kuzidi kwa kasi ya ukatili Jijini Mwanza kutajwa kuongezeka kumepelekea Kituo hicho kupokea watoto waliofanyiwa ukatili majumbani ambapo imevuka malengo kwa asilimia 25 ya mwaka ya kutegemea kuokoa watoto 40 na sasa wanaokoa watoto na kupokea wapatao 100 kwa mwaka.

Afisa, Emmanuel tangu kuanzishwa kwa kituo hicho mwaka 2011 kimeokoa zaidi ya watoto 120 waliounguzwa kwa moto na mpaka sasa watoto 94 wamerudi makwao na 27 ndiyo walio bakia kituoni hapo wakiendelea na matibabu na kusubilia kupewa elimu wazazi na walezi wao waliowafanya ukatili jambo ambalo huwaogopesha watoto hao wakati wakiambiwa kuchukuliwa kurudi majumbani mwao.
Picha za watoto waliokumbana na ukatili.

“Ukatiili huu upo kwenye majumba na kitendo cha watoto kufichwa majumbani baada ya kutendewa ukatili na kupatwa na majeraha husababisha wengi wao kupata ulemavu wa kudumu kutokana na kutelekezwa kwa kukosa Tiba ya haraka naya uhakika kwa majeraha waliyopata hali ambayo huwachukua muda mrefu kupona hasa wanapochukuliwa na Kituo hiki kuanza kufanyiwa utaratibu wa matibabu” alieleza.

Inasikitisha kwa mtoto huyu aliyekumbana na ukatili wa kucharangwa mikono kama ukataji muwa unavyokuwa.
Aliongeza kuwa Kauli mbiu ya Kituo hicho inaeleza kuwa “tunahitaji siku moja tuwe na Dunia huru dhidi ya Ukatili, watoto wawe salama na waone dunia ni sehemu sala kuishi kwa furaha na amani na sio kufanyiwa ukatili na kusababishiwa wao kuwa walemavu” imebainisha.

Afisa huyo ameitaka jamii kutambua sasa na kuanza kuchukua hatua na kumgusa kila mmoja kuanza kulishughulikia kukabiliana nalo ili kuwezesha kupunguza kasi na kumaliza kabisa kasi iliyoshamili ya ukatili wa watoto majumbani jambo ambalo halina budi kutolewa elimu na taarifa kwa jamii na viongozi wa serikali, vyama vya siasa na madhehebu ya dini maeneo mbalimbali vijijini na Wilayani kote. 


Picha hizi zinaonyesha madhara ya ukatili kupitia vipigo, kumwagiwa maji ya moto, kuchomwa moto, kufanyiwa ukatili kwa kutumia vitu vyenye ncha kali na kupigwa na vitu vizito sehemu mbalimbali za mwili.  

Jengo la kituo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.