ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, July 25, 2013

MNEC GACHUMA ALIVYOFUTURISHA WAISLAMU MWANZA

Mgeni rasmi wa hafla hiyo ya futari Mkuu wa Wilaya ya Nayamagana Baraka Konisaga alipata fursa ya kutoa shukurani na neno kidogo kwa wadau waliohudhuria hafla hiyo ya futari iliyoandaliwa na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa CCM wilaya ya Tarime 'Omary' Christopher Gachuma katika ukumbi wa new Mwanza Hotel na kuhudhuriwa na mamia ya waislamu na wageni wengine.

Mkuu huyo wa wilaya amewaasa wafanyabiashara kuepuka upandishaji bei wa bidhaa kipindi cha mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan kwani huwaumiza na kuwakomoa waislamuwenzao kitendo ambacho ni dhambi kwa Mwenyezi Mungu. 

Mashekhe, Mkuu wa wilaya pamoja na mwenyeji wa hafla hiyo ya futari MNEC 'Omary 'Gachuma wakijipatia chakula sahanini.

Marafiki wakiwa kwenye foleni ya maakuli walitumia muda huokupiga soga.

Mbunge wa Lorya Mhe. Lameck Airo akichukuwa chakula na pembeni yake ni Mzee wa Mwanza Charles Masalakulangwa.

Wadau wa PPF waliwakilishwa na Mr. Bandawe (mwenye miwani katikati)

Wadau toka chamani.

Mmoja kati ya Maafisa Uhusiano toka Ofisi za jiji la Mwanza Dr. Kaaya (kushoto) akijadiliana na mwendeshaji wa Hafla   hiyo ya Futari, Shekhe Hassan Kabete (kulia) na katikati ni Mkurugenzi wa Radio Metro Fm Hamran Batenga.

Kiduarisho hiki kiliwakilishwa na wadau hawa wa nguvu.

Meneja wa Airtel kanda ya Ziwa Ally Maswanya akiwa na wadau wake naye alijumuika kwenye kusanyiko hili la kirafiki zaidi.

Mwenyeji wa Hafla hiyo ya futari MNEC Gachuma (kulia) akiwa na Katibu wa BAKWATA mkoa wa Mwanza Shekhe Mohamed Bara.

Shekhe Mkuu wa Mkoa wa Mwanza (katikati) akiwa na mwenyeji wake MNEC 'Omary' Gachuma (kushoto) na wadau wengine wakipata futuru huku wakisikiliza yanayojiri.

Jumuiko la kirafiki.

Mara baada ya kufuturishwa dua fupi ilisomwa sambamba na shukurani kwa tukio hili ambalo limekuwa na ada ya kufanyika kila mwaka mara moja msimu huu..

Jumuiko.

Ni tukio jema...

Inshahlah Mwenyezi Mungu aendelee kumjalia muandaaji, Mweshimiwa Gachuma aendeleza ibada hii ambayo imekuwa chachu kwa Wanamwanza kudumisha amani na Upendo kwani huwakutanisha watu wa dini mbalimbali na kushiriki tukio la imani moja kiurafiki zaidi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.