ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, October 27, 2012

MATUMLA - MKENYA NDANI YA MTWARA HAPATOSHI

Bondia Rashid Matumla akipima uzito tayari kumkabili Mkenya.

Patrik Amot wa Kenya akipima uzito tayari kumkabili Matumla.

Maofisa wa TPBO wakitafakari masuala mbalimbali baada ya zoezi la upimaji afya kwa mabondia kufanyika mjini Mtwara.
Bondia Rashid Matumla wa Tanzania na Patrik Amot wa Kenya wanategemea kupanda ulingoni kesho katika ukumbi wa Makonde mkoani Mtwara.

Mabondia wote wamepima na kuwa na afya njema na wote kuwa katika uzani sawa wa kilo 73 kila mmoja.zoezi zima la upimaji liloendeshwa na katibu mkuu wa TPBO ibrahim kamwe na dr madono lilienda vema.

Pia kutakuwa na mapambano ya utangulii kati ya  bakari mohamed wa mtwara na abdala mohamed wa dsm katika pambano la ubingwa kg57

Pia kutakuwa na mapambano mengine mengi ya utangulizi kati ya mabondia toka Black Mamba ya Mtwara na mabondia toka Dar es salaam. kama Haruna Mnyalukolo atacheza na Ashraf Abdalah, Issa Matumla (mtoto wa Rashid Matumla) atacheza na Hamis Mtupeni,Hamis Ali Mkupa wa Mtwara atacheza na Ide Mnali katika pambano la raundi nane.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.