ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, June 17, 2012

LEO NI FAINALI YA AIRTEL RISING STARS


Vijana wanaoshiriki michuano ya Airtel Rising Stars wakiwa katika uwanja wa taifa jana kushuhudia mechi thidi ya Twiga Stars na Ethiopia, ziara hiyo imeandaliwa na Airtel yenye lengo la kuwafanya vijana kujifunza kutoka wacheza wa timu za mataifa.
Leo Jumapili 17/6/2012 vijana hao watashiriki michuano ya finali ya Airtel Rising Star itakayofanyika katika viwanja vya karume kuanzia saa sita mchana ambapo timu ya mbeya wasichana itachuana na timu ya Arusha wasichana kisha kufatiwa na mechi za wavulana ambapo Temeke itachuana na Arusha

Mshindi wa kwanza wa michuano ya Airtel Rising Stars atapata zawadi ya kombe, medali ya dhahabu na vitabu vyenye thamani ya shiling millioni moja wakati mshindi wa pili atapata medali ya fedha na vitabu vyenye thamani ya shilingi laki tano na mshindi watatu atapata medali ya shaba. Airtel pia itamzawadia mchezaji bora, golikipa bora, mfungaji bora na muamuzi bora wa mashindano

Na ili kuwapa mbinu zaidi za soka wachezaji, Airtel imeandaa kambi maalumu ya kimataifa ya mpira wa soka kwa nchi zinazoongea lugha ya kingereza ambayo itafanyika jijini Nairobi, kenya Agosti mwaka huu ambapo wachezaji sita watakaongara kwenye fainali hii ya leo watachaguliwa kushiriki,kambi hiyo itakuwa chini ya walimu wa soka kutoka klabu ya Manchester United ya Uingereza, Pia kikosi cha wachezaji kitachaguliwa leo katika fainali hii kushiriki michuano ya Afrika itakayojumuisha timu nyingine 13 za Afrika ambapo Airtel inafanya biashara . michuano hiyo pia itafanyika

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.