ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, April 3, 2012

VITUKO PICHANI: CUF NA BANGO LA MAITI YA MGOMBEA WA CCM TANGA

Wakuu.
Leo katika pitapita yangu maeneo ya kata ya Msambweni hapa jijini Tanga,nimekutana na kituko cha kusikitisha lakini kilichobeba ujumbe mzito kwa chama tawala. Ujumbe huo unasikitisha sana sana sana...kwa sababu umebeba picha ya umauti, Mimi kama mwanachama wa chadema, nimeshangazwa na namna wanachama wa CUF walio amua kutumia jeneza bandia na kikaragosi cha maiti kuonyesha hisia zao za kufurahia ushindi wa kata hiyo walioupata kwenye uchaguzi uliofanyika jana.

Haya ndio nimeya shuhudia kwenye upita njia wangu eneo la kata yaMsambweni ambayo ni mojawapo ya ngome za CUF kwa hapa jijini Tanga.

Kikaragosi cha maiti.

Bango pembeni mwa jeneza likiwa limebeba ujumbe mzito, nalo naona limebeba aina ya mchoko wa siasa za ushirika baina ya CUF na CCM.

Kwa mtazamo wangu , Cuf Hata kama wamekuwa na furaha ya namna gani ya kutetea kata yao hawakupaswa kusherehekea kwa kuweka picha ya mgombea wa ccm alieshindwa kwenye uchaguzi kwenye mfano wa jeneza bandia tena huku wakiweka sania ambalo kila anae pita njia anatupia pesa kama rambirambi.
Naomba kuwasilisha
From: "Mohamedi Mtoi"
Tanga, Tanzania

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.