
Jaji Mjema alihitimisha kusoma hukumu hiyo kwa kusema kwamba: "Kwa kuzingatia ushahidi uliotolewa na walalamikaji pamoja na upande na maelezo ya wa wadaiwa, mahakama hii inatupilia mbali mashtaka haya, na walalamikaji wanapaswa kulipa gharama zote za kesi hii".
"Kwa kweli huu ni ushindi wa kihistoria kwa nchi hii ya Tanzania. Lakini naamini kesi ni gharama na nitawafungulia kesi hawa watu ili walipe gharama zote nilizotumia. Nitakaa na mwanasheria wangu Tundu Lisu tuone gharama kiasi gani tumetumia", alisema Mbunge Kiwia huku akishangiliwa na mamia ya wafuasi wake.
Jaji Gadi Mjema akitoa hukumu hiyo leo amesema ushahidi uliotolewa na wakazi hao hautoshelezi na hivyo mahakama imemuachia huru mbunge huyo dhidi ya kesi iliyokuwa ikimkabili.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.