ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, November 19, 2011

BREAKING NEWS: MTOTO WA GADDAFI AKAMATWA

Serikali ya muda ya Libya inasema kuwa Saif al-Islam Gaddafi, mtoto wa kiongozi wa zamani wa nchi hiyo, amekamatwa.

Waziri wa Sheria wa serikali ya mpito, Mohammed al-Allagi, alisema kuwa Saif al-Islam amezuwiliwa karibu na mji wa Ubari, kwenye jangwa la kusini-magharibi mwa nchi.

Ripoti moja ilieleza kuwa hivi sasa amechukuliwa kwa helikopta kupelekwa Zintan, kaskazini mwa nchi.

Amekuwa akijificha tangu wapiganaji wa serikali ya mpito kuuteka mji mkuu, Tripoli, mwezi Agosti, na anasakwa na Mahakama ya Uhaini ya Kimataifa, kwa mashtaka ya uhalifu wa kivita.

CHANZO: bbc swahili.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.