Sekeseke limekuja tu mara baada ya askari wa Jeshi la Polisi waliokuwa katika Operesheni maalum inayoendeshwa ya kukamata pikipiki zenye makosa ya usalama wa barabarani, kumshambulia kwa kipigo askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).
Hata hivyo, wakati askari polisi wakimhoji huku pikipiki nyingine takribani kumi na tano zikiwa zimekamatwa, askari huyo wa JWTZ alimgeukia mmoja wao na kumuamuru kuvua kofia aliyokuwa amevaa kwa madai kwamba, ni mali ya JWTZ.
Amri ya askari huyo wa JWTZ ilipingwa na askari polisi, ambao walifura kwa hasira nakuanza kumpa kipigo.
Kitendo hicho kiliwaudhi wananchi waliokuwa wakifuatilia tukio hilo wakidai kuonewa mara kwa mara na askari hao, ambao waliingilia kati na kuanza kuwashambulia askari hao kwa mawe.
Askari hao walipoona wamezidiwa, walikimbilia katika kituo cha polisi cha Market na wananchi hao waliendelea kuwashambulia kwa mawe.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Simon Sirro, alithibitisha kuwapo operesheni ya kukamata pikipiki na kusisitiza kuwa zoezi litaendelea.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.