Mshambuliaji wa Yanga, Jerry Tegete alianza kuwainua mashabiki wa Mwanza kwa kufunga bao la kwanza dakika 45 baada ya kuwatoka mabeki wa Ilala kabla ya kufumua shuti kali lililojaa wavuni. Dakika 45 za kwanza, Mwanza ilicheza soka ya kiwango bora kwa kufanya mashambulizi mara kwa mara langoni mwa Ilala ambayo ilionyesha udhaifu sehemu ya kiungo na kutoa mwanya kwa wapinzani wao kucheza kwa nguvu.
Kipindi cha pili kilianza kwa Mwanza kuliandama lango la Ilala na juhudi zao zilizaa matunda dakika 57 baada ya Tegete kufunga bao la pili kwa mkwaju wa penalti kufuatia mchezaji Erick Mawala kumfanyia madhambi Maregesi Mwangwa katika eneo la hatari akielekea kufunga.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.