Polisi amesema kuwa jirani yake aliuona mwili wake mlangoni kwake akiwa amejifunga skafu na kamba shingoni wkati wa saa nane usiku na ndipo tu aliita watu wa huduma za dharura. Uehara alikimbizwa hospitali ambako madakari walidhitisha kuwa alikwishakufa.
Kwa mujibu wa mtandao wa kihabari wa japantoday , Uehara ni mmoja wa watoto 10 waliozaliwa nyumba moja anayetokea mkoa wa Kagoshima, jambo ambalo si la kawaida sana nchini Japani (Watoto wengi katika familia moja) na kipaji chake kilijibainisha wakati akifanya kazi ya uhudumu katika klabu moja ya starehe, wakati huo alikuwa na miaka 18.
Hapo alianza kuonekana kwenye majarida ya wanaume akiyapamba kwa picha zake zilizowafanya wanaume wengi hususan vijana kuyanunua kwa wingi na baadaye alifahamika kama “Malkia” miongoni mwa mashabiki wake.

Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.