Serikali mpya ya Rais wa Ivory Coast Alassane Ouattara inaandikisha wanajeshi wapya kuboresha hali katika mji mkuu wa kibiashara Abidjan baada ya miezi minne ya ghasia za kisiasa. Habari zaidi zinasema maisha yameanza kurudi katika hali ya kawaida ikiwa ni chini ya wiki moja baada ya kukamatwa kwa rais wa zamani nchini humo, Laurent Gbagbo.Katika hatua za awali Raisi Ouattara alikutana na Mkuu wa majeshi Jenerali Phillipe Mangou katika hoteli ya Golf ya Abijan.Hivi sasa baadhi ya wanamgambo wa Ouattara wanayo nafasi ya kujiunga na serikali mpya ya Ouattara kama wanajeshi na polisi.
Mwalimu wa mafunzo katika kundi jipya la Repuplican Forces nchini Ivory Coast, Yaya Cisse, anasema "hawa ni raia ambao watapatiwa mafunzo kuwa wanajeshi kamili huku wale ambao wanataka kuwa polisi wataendelea na Wale ambao wanataka kuacha, tutawaruhusu kufanya hivyo"
Kuweka sawa huduma za usalama nchini Ivory Coast ni sehemu kubwa ya kurudisha tena ushwari katika mji mkuu wa kibiashara ambapo Rais Ouattara anataka kuanza haraka uuzaji wa kakao nje ya nchi, kufungua tena mabenki na kukufua tena viwanda ili uchumi wa nchi usonge mbele.
Hata hivyokamatakamata bado inaendelea nchini humo , ambapo wafuasi sugu wa Gbagbo waliopo jeshini wamekuwa wakitiwa kwenye mikono ya dola...
Fahamu tofauti kati ya Eid ul-Fitr na Eid ul-Adha
-
Ingawa baadhi ya waislamu hufuata kalenda iliyowekwa ya mwezi na wengine
hutumia uchunguzi wa unajimu kutangaza kuonekana kwa Mwezi mpya, Waislamu
wengi hu...
RAIS SAMIA AFTURISHA WATOTO KIKOMBO DODOMA
-
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe.
Mwanaidi Ali Khamis akigawa iftar kwa mmoja ya mtoto anayelelewa katka
Makao ...
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.