ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, March 24, 2011

KUTOKA PEMBA - KUTANA NA MPEMBA HALISI.

Kama u-mmoja kati ya wahudhuriaji wa mara kwa mara wa mikutano na makongamano mbalimbali hata ile ya kisiasa jina 'Mpemba Asili' bila shaka utakuwa unalipata.Huyu ni mshairi kutoka Wete Pemba kijiji cha Ole nae akiishi na kufanya kazi mjini Dodoma kama mwelimishaji kwa njia ya mashairi kwa kuzingatia majanga kama Ukimwi, Rushwa, Umaskini, Madawa ya kulevya, Afya bora kwa jamii, Utunzaji mazingira na Kuelimisha wa Tanzania kujitambua.

Anasema amejitahidi sana kuwarithisha vijana wengi kipaji alichonacho cha utunzi wa ushairi lakini wengi imekuwa UTATA...

MPEMBA ASILI ANAKETI NA WATU WA RIKA ZOTE USISHANGAE KUMWONA KWENYE VIJIWE VYA:-

WATOTO = kujua ladha ipendwayo na njia fupi ya kuifundisha haraka jamii ikaelewa.

VIJANA = dunia na maendeleo yake.

MASELA = misemo ya kisasa ya mtaani inayopenyeza ujumbe kirahisi.

WAZEE = hekima, busara na lugha fasaha.

Huyo ni 'Mpemba Halisi'

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.