Umoja wa makanisa jijini mwanza jana jioni umefunga rasmi mkutano wake mkubwa wa injili uliojulikana kwa jina 'D-Change Festival'. Kusanyiko hilo lilihusisha wanamuziki wa injiri akiwemo Solomoni Mukubwa, Anastazia Mukabwa, kundi la The Fielder-Marshals pamoja na Mhubiri na Muimbaji mkongwe Askofu Ben Bahati.Solomon Mukubwa akiwaimbisha wananchi waliofurika kwa wingi viwanja vya Furahisha, moja ya nyimbo zake.
Askofu Ben Bahati akiwaongoza watu walijitokeza kwa wingi kwenye viwanja hivyo vinavyopatikana kirumba jijini Mwanza, katika sala ya toba kama ishara ya kumpokea YESU kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yao.
Anastazia Mukabwa akiimba wimbo wa KIATU KIVUE mbele ya umati wa wakazi wa Mwanza,na kisha akaimba wimbo wake wa "Anayekudharau siku moja atakusalimia kwa Heshima" uliionekana kuwasisimua wengi uwanjani hapo.
Umati wa watu ulijitokeza kusikiliza habari njema za Kristo katika viwanja vya Furahisha jijini Mwanza.
Kundi la The Field-marshals toka Kenya likimsifu MUNGU katika siku husika.
RAIS SAMIA AFTURISHA WATOTO KIKOMBO DODOMA
-
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe.
Mwanaidi Ali Khamis akigawa iftar kwa mmoja ya mtoto anayelelewa katka
Makao ...
it was very Poweful,Hop this year many Crusades will be done on those Grounds.
ReplyDelete