ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, April 12, 2023

DC KALLI AKABIDHI GODORO GEREZA LA (BANGWE)KIGOMA.


Na. Sebastian Salum.

Mkuu wa wilaya ya kigoma Salum Kalli, amekabidhi magodoro 35,katika gereza la wilaya Bangwe kigoma.


Akikabidhi magodoro hayo yaliyotolewa na mkurugenzi wa Radio Joy bw.Mwenge Muyombi.




Mh.Kalli ameiasa jamii, na taasisi mbalimbali, kuendelea kujitoa ili kuimaliza changamoto ya magodoro, katika gereza hilo, ikiwa ni sehem ya jamii ya kigoma, na sehem ya mafunzo ya tabia kwa wananchi.


Kwa upande wake Mratibu mwandamizi wa magereza, Bakari kasenga. ambae ni Mkuu wa gereza hilo, amemshukuru Mkuu huyo, pamoja na Uongozi wa Radio Joy,kutatua changamoto ya upatikanaji wa magodoro,kwa kuwakabidhi jumla ya godoro 35 mbapo awali Walipokea pia godoro 30 kutoka Uongozi wa Radio Joy.

Mkuu huyo ametumia tukio hilo, kutembelea kiwanda kidogo cha utengenezaji wa samani mbali mbali za nyumbani, ikiwa ni sehem mojawapo ya mafunzo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.