ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, September 21, 2022

MAAFISA TARAFA NA WATENDAJI WA KATA IRINGA MABALOZI WAPYA UTALII HIFADHI RUAHA.

 

Mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo akiongea na maafisa Tarafa na watendaji wa Kata walioenda kufanya utalii katika Hifadhi ya Taifa ya Ruaha juu ya umuhimu wa kuendelea kuitangaza hifadhi hiyo
Mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo kushoto,kaimu Afisa Tarafa Pawaga Emmanuel Ngabuji katika na kulia ni mwandishi wa habari Fredy Mgunda wakiwa kwenye utalii katika hifadhi ya Taifa ya Ruaha 
Baadhi ya watendaji na Maafisa Tarafa wakifanya utalii wa Daraja la kamba lililopo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha ikiwa ni moja ya vivutio vilivyomo ndani ya hifadhi hiyo
Baadhi ya watendaji na Maafisa Tarafa wakifanya utalii wa Daraja la kamba lililopo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha ikiwa ni moja ya vivutio vilivyomo ndani ya hifadhi hiyo
Baadhi ya watendaji na Maafisa Tarafa wakifanya utalii wa Daraja la kamba lililopo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha ikiwa ni moja ya vivutio vilivyomo ndani ya hifadhi hiyo


Na Fredy Mgunda,Iringa.

Maafisa Tarafa na watendaji wa kata zote za wilaya ya Iringa wameahidi kuwa mabalozi wa kuvitangaza vivitio vya utalii vilivyopo katika hifadhi ya Taifa ya Ruaha ili kuongeza chachu ya ongezeko la watalii katika ukanda wa nyanda za juu kusini ikiwa nu sehemu ya kuunga mkono jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan katika kusisimua uchumi kupitia seta hiyo muhimu nchini.

 

Wakizungumza wakati wa ziara ya Utalii ya maafisa Tarafa na Watendaji kutoka wilaya ya Iringa iliyoratibiwa na mkuu wa Wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo, walisema kuwa wamefurahishwa na namna hifadhi hiyo ilivyokuwa na vivutio vingi ambavyo vipi ndani ya hifadhi hiyo.

 

Emmanuel Ngabuji ni kaimu Afisa Tarafa Pawaga alisema kuwa hifadhi ya Taifa ya Ruaha imejaliwa kuwa na vivutio vingi ambavyo mtalii akifika katika hifadhi hiyo atafurahia na hatatamani kuongoka kutoka kuwapata furaha awepo kwenye hifadhi hiyo.

 

Ngabuji alisema kuwa watendaji wengi imekuwa mara yao ya kwanza kutembelea hifadhi ya Taifa ya Ruaha hivyo asilimia kubwa wamejipanga kwenda kutoa elimu ya utalii kwa wananchi wanaowaongoza huko katani.

 

Alisema kuwa amejipanga kuhakikisha wananchi wa tarafa ya Pawaga wanaandaa Safari maalumu ya kwenda kutembelea hifadhi ya Taifa Ruaha ili waweze watoto na wananchi wengine kuupenda utalii wa ndani.

 

Ngabuji alisema kuwa wanamshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa namna ambavyo amekuwa akiutangaza utalii wa ndani kupitia filamu ya Royal Tour ambayo imeanza kuleta matokeo chanya ya ongezeko la watalii nchi na watalii wa ndani kuongezeka kutembelea vivutio mbalimbali.

 

Stella makali na Aunt Mbilinyi ni watendaji wa kata walisema kuwa wamefurahi kufanya utalii katika hifadhi ya Taifa ya Ruaha baada ya kuona namna ambavyo mnyama Simba anavyofanya mapenzi jambo ambalo hawajawahi kuliona toka wanzaliwe hivyo inawafanya watafute muda mwingine wa kwenda kufanya utalii katika hifadhi hiyo.

 

Walisema kuwa wamefurahia kutembelea hifadhi hiyo kwa namna ambavyo wameona wanyama mbalimbali na wanavutia kiasi kwamba ukiwa katika hifadhi hiyo utakuwa na furaha muda wote kwa namna ambavyo vivutio vingi vilivyopo ndani ya hifadhi ya Taifa ya Ruaha.

 

"Tumerithishwa,Tuwarithishe tuungane kwa pamoja kuokomeza ujangili katika hifadhi yetu ya Ruaha iliyopo mkoa wa Iringa ili hata watoe watu waje waone wanyama na vivutio vilivyomo hifadhini"alisema makali

 

Walisema kuwa wanamshukuru mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo kwa kuwaandalia Safari ya kwenda kutembelea hifadhi ya Taifa ya Ruaha kwa watendaji wa kata na maafisa Tarafa jambo ambalo limefanyika kwa mara ya kwanza na limekuwa kivutio kikubwa cha kuendelea kuvitangaza vivutio vilivyopo katika wilaya ya Iringa.

 

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo alisema kuwa lengo la kuwapeleka maafisa Tarafa na watendaji kutalii katika hifadhi ya Taifa ya Ruaha ni kutambua umuhimu wa utalii na namna ambavyo wanaweza kuwalinda wanyama pori wasitoweke ili kuwaliaisha wananchi wengine.

 

Moyo alisema kuwa maafisa Tarafa na Watendaji wa Kata kutembelea hifadhi ya Taifa ya Ruaha kunaongeza chachu ya ongezeko la watalii katika ukanda wa nyanda za juu kusini ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan katika kusisimua uchumi kupitia seta hiyo muhimu nchini.

 

Alisema kuwa viongozi wa serikali za vijiji kata na Tarafa wanauwezo mkubwa wa kutoa elimu kwa wananchi juu ya umuhumu wa kufanya utalii wa ndani na ukaleta tija kwa taifa na wilya ya Iringa kwa ujumla wake.

 

 

 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.