ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, September 23, 2012

BREAKING NEWS: KUDHARAU AMRI YA MAHAKAMA KWASABABISHA KIKAO CHA UCHAGUZI CHADEMA KUMPATA MGOMBEA UMEYA NA NAIBU MEYA KUVUNJIKA MWANZA

KIKAO cha Kamati ya Utendaji cha Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimevunjika baada ya kukaidi amri ya halali iliyotolewa na Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza iliyokuwa imeelekeza kumrejeshea uanachama diwani wa Kata ya kitangiri Henry Matata na aweze kushiriki katika kinyang’anyilo cha kumchagua Meya na Naibu Meya kutoka CHADEMA na kusababisha baadhi ya wafuasi wa chama hicho kuingilia kati na kuwatawanya wajumbe wake kwa nguvu na kuwatoa nje ya ukumbi.

Polisi wakizozana na walinzi wa kikao hicho cha CHADEMA 
Vurugu hiyo iliyotokea majira ya saa 6 :42 za mchana katika ukumbi wa hoteli ya Ladson iliyopo maeneo ya Bwiru Wilayani Ilemela ambapo kundi kubwa la vijana wanaodaiwa ni wafuasi wa chama hicho wakitoka kata ya diwani aliyeenguliwa uanachama Henry Matata walipovamia na kufanya vurugu kubwa na kusababisha hali kuwa mbaya na viongozi hao kuwaita Polisi ambao awali walishauri viongozi hao kuahilisha kikao hicho kutokana na kuwepo ukiukwaji wa amri hiyo ya Mahakama Kuu ya Kanda ya Mwanza.

Maafikiano hayakupatikana...
Kamanda wa Polisi Wilaya ya Ilemela (OCD) Debora Magrigimba alipofika eneo la uchaguzi  saa 4:00 asubuhi  akiwa ameambatana na Mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai wa wilaya Magesa hiyo wakiwa na barua ya Mahakama Kuu iliyosainiwa na Jaji Sumar, ya tarehe 14 septemba mwaka 2012 iliyokuwa inaelekeza chama hicho kumshirikisha mwanachama wake huyo kuendelea na harakati zake za kuwania nafasi ya Meya hadi hapo kesi ya msingi itakapomalizika katika Mahakama hiyo.

Mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai wa wilaya Magesa (aliyenyoosha mkono kulia) licha ya kuwasihi wadau hao wa CHADEMA kufuata amri ya mahakama hakuna aliyetii....

Mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai wa wilaya ya Ilemela Magesa akiwa na  Kamanda wa Polisi Wilaya ya Ilemela (OCD) Debora Magrigimba wakijadiliana huku wadau wanaoongoza  kikao cha Uchaguzi huo mdogo wa CHADEMA nao wakishikilia msimamo wao kutoruhusu jina la diwani Henry Matata kuingizwa kwenye orodha ya majina ya wagombea uwakilishi nafasi ya U- Meya.

Polisi hao walilazimika kuondoka mara baada ya viongozi wa uchaguzi huo kukaidi amri ya mahakama.
 Utata ulizuka pale viongozi wa CHADEMA akiwemo Mbunge wa Jimbo la Ilemela Highness Kiwia na Madiwani waliokuwa waalikwa katika kamati hiyo ya Utendaji ya Wilaya na kushikilia msimamo wa kutoingiza jina la diwani Matata kufanyiwa usaili ili ashiriki kugombea nafasi ya Meya.
Kundi la vijana wanaosadikika kumuunga mkono diwani Henry Matata walivamia kikao hicho na kuanza kuwashambulia wajumbe waliokuwa kwenye kikao hicho cha uchaguzi hali iliyosababisha polisi kurejea eneo la tukio kutuliza ghasia zilizozuka nao wakafanikiwa kumnasa mtu mmoja tu kati ya mamia walileta vurugu.

Kundi la vijana likitinga lango la kikao cha uchaguzi wa CHADEMA kufanya vurugu.

Aliyekuwa meya wa jiji la Mwanza kupitia CHADEMA Mh. Manyerere (mwenye shati la bluu akitafakari jinsi ya kutoka kwenye chumba cha mkutano) huku akiwa amezungukwa na baadhi ya wajumbe nao wasijuwe watatokaje ndani ya chumba hicho mala baada ya kuzingirwa na Kundi la vijana walioleta vurugu kikao hicho kisiendelee.

Ilibidi polisi warejee eneo la tukio mara baada ya kupata taarifa za machafuko na hapa lilitaka kutokea varangati baina ya diwani Matata wa kata ya Kitangili (anayeamuliwa) na diwani Manyerere mara baada ya kurushiana naneno huku maafisa wa jeshi la polisi wakizuia.

 Mwenyekiti wa CHADEMA wilaya ya Ilemela Yunus Chilongozi amewataka wanachama wa chama hicho kuwa watulivu...
Kijana huyu ametiwa nguvuni kuhusishwa na sakata hilo...

Hali ya usalama iliimarishwa hatimaye wajumbe mmoja baada ya mwingine walitoka ukumbini na kutawanyika.

Mbunge wa wilaya ya Ilemela jijini Mwanza  Highness Kiwia akitoka eneo la uchaguzi huku akipewa ulinzi.


Mbunge Highness Kiwia akizungumzia sakata hilo mbele ya ofisi za CHADEMA wilaya ya Ilemela ... Sikiliza...


Sikiliza alichosema diwani Henry Matata kuhusu sakata hilo na kushutumiwa kwake kuhusishwa na vurugu hizo, yeye kasema vijana hao ni wake.


Hivi karibuni madiwani wawili Henry Matata wa kata ya Kitangili na Bw. Adam Chagulani wa kata ya Igoma walitinga mahakamani kupinga uamuzi wa kuvuliwa uanachama na Kamati kuu ya CHADEMA wakidai kuwa uamuzi wa kuwatimua ulikiuka taratibu za chama hicho na katiba.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.