ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, July 1, 2013

HAIJAWAHI KUTOKEA KAMA HII YA TIGO NKABAaaaaa JIJINI MWANZA - SHOW YASITISHWA KWAKUHOFIA USALAMA

Diamond The Platnum akikisanukisha ndani ya show ya kubwa iliyopata mashabiki ambao idadi yao haijawahi kutokea ya Tigo Nkabaa uwanja wa CCM Kirumba Mwanza na kupata shangwe za kutosha. 

We wachaaaaa....!!

The Platnum mwenyewe.

Shangwe za hapa ilikuwa balaaa.. toka kwa mashabiki kwenda kwa supa staa huyu.

Chekshia magoli ya basketball yalipogeuka kuwa majukwaa.

Ney wa Mitego alipata shangwe za kutikisa...

Ngosha ze Swagz' Fid Q

On the one & two.

Roma akisalimia watu wake ambapo dimba la CCM Kirumba lilitapika kwa kuwa na mashabiki mizunguko yote...

Siwasikiiiii.

Seksheni ya Chomaz na Dada Dory.

Jirambeeeee.

Rich Mavoko... akilimeneji stage.


Recho toka THT.

Full house full nyomiiii....watu zaidi ya elfu 40.

Recho dance.

Stiko jukwaani...

Jinsi hali ilivyokuwa ikisonga mbele nao mashabiki kusogea zaidi kulifikia jukwaa askari walitumia mbwa kusogeza mashabiki wakati huo milango ikafungwa hakuna ruhusa kuingia watu tena. 

Hata show iliposimama mashabiki waliendelea kuwapo ndani ya uwanja wakidhani ni mkwara tu show ingeendelea kumbe ndiyo bye bye ya Nkabaaaa...

Afande Kotecha akiwaamuru mashabiki kuondoka sasa uwanjani kwani hali ya usalama siyo nzuri na mashabiki wameshindwa kutulia.

"Sasa tumetuliaaaa...." Ni kama kauli za mashabiki walioshuka toka majukwaani na kuketi nyasini wakilizonga jukwaa ili wapate kuendelea na burudani.

Afande Kotecha akimwamuru Diamond kushuka ili pasitokee maafa.

Njia iliwekwa sawa.....kisha mnyamwezi  the Platnum akapanda kwenye gari maalum na kusepa...

Hata kutoka kiwanjani napo kulikuwa inshu...

Kazi kweli kweli dimbani CCM Kirumba Mwanza Tanzania, hakika hii ni historia nyingine mpya imewekwa jijini hapa.
By G. Sengo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.