ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, October 9, 2017

INSIGHT YASHEREHEKEA MIAKA 10 TANGU KUANZISHWA KWAKE

Allen Komba, Mfanyakazi wa Kampuni ya masuala ya Ulinzi ya Insight (Zamani Warrior Security) akipokea zawadi kutoka kwa Jacqui Sugden akiwa kama mmoja wa wafanyakazi aliyeitumikia kampuni hiyo tangu kuanzishwa kwake mwaka 2007. Zawadi hiyo ilitolewa wakati wa kuadhimisha miaka 10 ya Insight ambayo ni Kampuni inayoaminika zaidi kwenye masuala ya ulinzi na Usalama Afrika Mashariki na Kati, katika hafla ya chakula cha jioni iliyofanyika katika hoteli ya Sea Cliff mwishoni mwa juma jijini Dar es salaam.


Oktoba 2017, Dar es Salaam: Kampuni ya WS Insight ambayo hapo awali ilijulikana kama Warrior Security jana usiku iliandaa chakula cha jioni katika hafla ya kuadhimisha muongo mmoja (miaka10) wa mafanikio, ikiwa ni miongoni mwa kampuni inayoaminika katika utoaji wa huduma bora za ulinzi na usalama ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.

Tukio hilo la chakula cha jioni lilifanyika jana usiku katika Hoteli ya Sea Cliff na liliwakutanisha zaidi ya wageni 100 kutoka katika sekta mbalimbali ambao waliburudishwa vilivyo na mchekeshaji mahiri kutoka Kenya, Eric Omondi. Pia kulikuwapo na zawadi kwa wafanyakazi ambao wameitumikia Kampuni hiyo kwa takribani miaka 10 sasa.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mtendaji na mmoja wa waanzilishi wa WS Insight, Tony Sugden alisema, “Baada ya kutimiza miaka 10, ninajivunia kusema kwamba hii ni kampuni yetu. Kampuni ilianza kufanya shughuli zake mkoani Arusha mwaka 2006 ambapo kwa sasa imeajiri watu 1,500 kwa Tanzania pekee na ina jumla ya wafanyakazi 7,000 kwa nchi tano ambazo tunatoa huduma.”
“Ws Insight ilianzishwa kwa lengo la kutengeneza Mazingira salama ya kuwawezesha watu na biashara kuwa salama. Hilo ndilo jambo ambalo linatufanya kila wakati kufikiria majibu wanayohitaji wateja wetu na tunatimiza hayo yote kwa kufanya kazi zetu kwa kuzingatia uzoefu na ujuzi jambo ambalo linaongeza ufanisi katika upatikanaji wa taarifa kila wakati. Hakuna yeyote anayeweza kujilinganisha nasi kwa ufuatiliaji.”
Kampuni yetu iliyoanzishwa Tanzania, imefanikiwa kujitanua hadi Sudan Kusini mwaka 2008, pia nchini DRC mwaka 2011. Zambia ilifika mwaka 2013 na Kenya mwaka 2014 huku tukibadili jina kutoka Warrior Security hadi kuwa WS Insight mwezi Machi mwaka huu. Kampuni ya Insight Group kwa sasa ina mapato ya Dola za Marekani milioni 35 kwa mwaka.
Wateja wetu ni pamoja na Tier One Mining, Oil & Gas, UN, Mashirikia yasiyo ya kiserikali (NGOs), Serikali na taasisi za kibiashara ambazo zipo katika mazingira magumu duniani.

Mambo ya muhimu kwa wahariri

Kuhusu WS INSIGHT
WS Insight (Zamani Warrior Security) ni kampuni ambayo imejikita kwenye utendaji kazi (ikiwa na mapato ya Dola 35 milioni huku ikiwa imeajiri zaidi ya wafanyakazi 7,000). Pia ina uzoefu wa miaka 10 ya utoaji huduma zake kwa kiwango cha juu kwa wateja wetu barani Afrika zikiwamo nchi za DRC, Sudan Kusini, Zambia, Kenya na Tanzania. WS Insight imekuwa ikifanya kazi kaztika maeneo ambayo inayafahamu vyema katika Afrika Mashariki na Kati ikihudumia wateja wakiwemo Tier One Mining, Oil & Gas, US State Department, USAID, UN, ofisi za kidiplomasia, asasi za kimataifa, pamoja na taasisi mbalimbali za kibiashara.
Kampuni ilianza ikiwa na Tony Sugden na Ashton Towlr na Mkugenzi wa Tanzania akiwa Matt Merrick.

Wasifu wa Tony Sugden –Mkuruenzi Mtendaji na Ofisa Mkuu Mtendaji wa Kampuni (Group)
Ni miongoni mwa waanzilisi wa Warrior Security mwaka 2006. Tony amekuwa na uzoefu kwa zaidi ya miaka 15 kwenye biashara ya ulinzi kwa ukanda wote wa Afrika Mashariki na Afrika na Kati. Amekuwa akiongoza zaidi ya watu 5,000 na kuendesha programu za mafunzo, hatua mbalimbali na mifumo mikubwa na midogo kwa wateja wakiwamo Idara ya Ikulu ya Marekani, Taasisi za UN, mashirika ya kibiashara na pia ya watu binafsi.

Wasifu wa Ashton Towler biography –Mkurugenzi na Mkuu wa Fedha
Ni mwanzilishi wa Warrior Security mwaka 2006. Ashton ni mwanachama wa Taasisi ya Chartered Accountants nchini Uingereza na Wales. Ashton amepata mafunzo ya kompyuta na kupata shahada ya kompyuta daraja la la kwanza la juu (Hons) kutoka Chuo Kikuu cha Manchester. Baada ya kuhitimu Ashton alifuzu kuwa mhasibu cheti cha taasisi hiyo ya juu ya uhasibu na kufanya kazi na Arthur Andersen jijini London na baadaye akajiunga na CDC Group ambapo alitekeleza majukumu mbalimbali ya uwekezaji kwa miaka miatano ambapo alifanikiwa kufanya uwekezaji katika ukanda wa Afrika Mashariki na Afrika Magharibi.
 Ashton amepata uzoezfu mkubwa katika asekta mbalimbali na kwenye mashirika mbalimbali  na kukuza mipango ya maendeleo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.