ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, October 3, 2017

IDARA YA MAJI SENGEREMA YAZIWEKA ROHO ZA WANANCHI REHANI.

VIDEO KUWAJIA HIVI PUNDE.


WAKAZI WA MJI WA SENGEREMA WILAYANI HUMO WAMEILALAMIKIA MAMLAKA YA MAJI KATIKA HALMASHAURI HIYO KWA KUKOSA MAJI NA KUPELEKEA KUTUMIA MAJI YA LAMBO AMBAYO YANAWEZA KUPELEKEA KUHATARISHA AFYA KWA WAKAZI HAO
 Wakizungumza na Jembe Fm wakazi hao wamesema ni zaidi ya wiki mbili sasa wanatumia maji ya lambo ambayo si safi na salama kwa matumizi ya binadamu kwakuwa yamekuwa yakitumiwa kunyweshea mifugo mbali mbali,kufulia na hata kuoshea magari

Naye diwani wa Ibisabageni mh:Jumanne Masunga amesema kuwa maji imekuwa kero kwa wananchi kutokana na mradi mkuwa wa maji Nyamazugo kuzinduliwa hivi karibuni na mh;Rais Magufili,na kishahuri mamlaka husika kutanzua kero hiyo kwa wananchi

Akizungumza kwa njia ya simu meneja wa mamlaka wa maji wilayani sengerema bwana CHRISTOPHAR KIONE  amesema kuwa  juhudi za kutanzua tatizo hilo zinaendelea kuwanyika  na kuwataka wananchi kuwa na subira wakati wowote tatizo hilo litakwisha

Kutokana na kero hiyo bei ya maji  imepanda kutoka shilingi miambili kwa ndoo hadi shilingi miatano kwa ndoo na maji hayo si safi na salama

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.