ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, June 24, 2014

HII HAPA VUNJA JUNGU KALI KULIKO ZOTE KATI YA ZILE ZINAZO KUJA.

NA PETER FABIAN, MWANZA.
KIDUMU na Bendi yake ya Bodaboda kutoka nchini Kenya atamba kutoa burudani ya nguvu ili kusuuza mioyo ya mashabiki wa muziki dansi wakati wa usiku wa vunja jungu ndani ya mpambano wa bendi tatu jijini Mwanza.

Akiongea nami kwa njia ya simu kutoka jijini Nairobi nchini Kenya, Kidumu ambaye ni mwanamuziki anayemiliki bendi hiyo alisema kwamba, mashabiki wa Jiji la Mwanza wasiwe na wasi kwakuwa lugha ya Kiswahili haimpatii shida na atapiga nyimbo zake zikiwemo alizoimba kwa lugha hiyo.
“Nakuja Jiji la Mwanza kutoa burudani na siyo kuuza sura hivyo mashabiki wangu wataona na kushuhudia jinsi bendi yao ya bodaboda ikifanya vitu adimu jukwaani na hakuna ubishi kazi itafanyika ili kuweka heshima kwa mashabiki,”alisisitiza.

Aidha mwanamuziki huyo alieleza kuwa hana wasiwasi na kupambanishwa na bendi yayote ya muziki katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kwani anajiamini kwa kazi za kutoa burudani kwa mashabiki hivyo naomba sapoti kutoka kwao ili kwani bila wao hakuna muziki jukwaani.

 “Tumejipanga na mashabiki watakaofika watapata ladha na vionjo tofauti kutokana na show itakayofanywa na Bodaboda bendi, lakini natumai Malaika bendi na Super Kamanyola nao wako vizuri na wamejipanga ili kuona nani zaidi kwenye mpambano huo,”alisema mwanamuziki huo.

Kwa upande wake meneja wa burudani wa Villa Park Resort Ramadhan Maganga alisema kwamba bendi ya hizo tatu za Bodaboda chini ya kiongozi wake Kidumu kutoka nchini Kenya, wakati bendi ya Malaika itaambatana na mkali wake Christian Bella toka jijini Dar es salaam na Super Kamanyola wenyeji wa jijini watakuwa chini ya wakali wao Benovila Anthon, Roy Makuna na Rashidi Mwezingo.


Maganga amewataka mashabiki “wafike  kujionea cheche za nani mkali zaidi wa bendi na madj siku hiyo katika usiku wa vunja jungu ambao tumeandaa mambo makubwa ikiwa ni pamoja na uboreshwaji wa huduma ya vyakula na vinywaji pamoja na ulinzi wa hali ya juu kwa mali watakazokuja na kuziacha nje ikiwemo usalama wa magari kwa asilimia 100 na hakuna vurugu,”alisisitiza.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.