ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, October 2, 2013

AIRTEL YAKABIDHI VITABU VYA MILIONI 10 SEKONDARI 4 MKOA WA DODOMA

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dr Rehema Nchimbi akiwakabidhi msaada wa Vitabu  vilivyotolewa na Kampuni ya simu ya Airtel Wanafunzi Mariamu Hamisi na Theodory Raymond wa kidato cha kwanza shule ya Sekondari Dodoma wengine katika picha nyuma ni meneja mauzoAirtel Dodoma Saidimu Ngaleson na Mkuuwa Shule hiyo Maico Masala
Mkuu wa Shele ya Sekondari ya Kibakwe  ya Wilaya ya Mpwapwa Mkoan i Dodoma Augustine Senya (kulia) akipokea msaada wa vitabu kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dr Rehema Nchimbi msaada huo wa vitabu ulitolewa na Airtel kwa Sekondari tano za Mkoa wa Dodoma, wengine nyuma wanaoshuhudia ni kutoka kushoto ni Hedrick Werner Afisa masoko Airtel Kanda ya kati na  Saidimu Ngaleson Afisa mauzo Airtel Mkoa Dodoma
Afisa Elimu Taaluma Wilaya ya Chamwino Mkoani Dododma Hamisi Mapoto (kulia) akipokea msaada wa Vitabu kwa niaba ya Mkuu wa Shule ya Sekondari Itisso na Mkuu wa Mkoawa Dodoma Dr Rehema Nchimbi (kushoto) msaada huo umetolewa na kampuni ya simu ya Airtel,nyuma ni meneja mauzoAirtel Dodoma Saidimu Ngaleson
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dr Rehema Nchimbi (kushoto) akikabidhi msaada wa vitabu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Bihawana Dodoma Crispin Mtesigwa (kulia)  uliotolewa na Airtel kwa kwa shule hiyo jana ,wengine nyuma toka kushoto ni   meneja mauzo Airtel  Mkoa wa Dodoma Saidimu Ngaleson na mwalimu Helbet Ngusulwa
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rehema Nchimbi (kushoto) akimkabidhi msaada wa Vitabu vilivyotolewa na Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel kwa shule tano za Sekondari za Mkoa wa Dodoma Kaimu Afisa Elimu taaluma Wilaya ya Kongwa Mkoani Dodoma Sarael Jonas ,wengine ni  meneja mauzoAirtel Dodoma Saidimu Ngaleson (kulia) na Afisa masoko Airtel kanda ya kati Hendrick Werner
Airtel yakabidhi vitabu vya milioni 10 sekondari 4 mkoa wa Dodoma
•       Airtel yakabidhi vitabu kwa shule za sekondari Bihawane, Kibakwe, Itiso na Ndido mkoani Dodoma 
Katika muendelezo wa kuhakikisha inatoa huduma zilizo bora kwa jamii nzima, Kampuni ya mitandao ya simu za mkononi ya Airtel kupitia mradi wake wa shule yetu imefanikiwa kutoa vitabu vya kiada kwa shule mbalimbali zilizopo katika manispaa ya Dodoma.

 Miongoni mwa shule zilizonufaika na mradi huo ni pamoja na Bihawane, Kibakwe, Itiso na Ndido zote zikiwa ni shule za sekondari katika mkoa huo.

 Akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi vitabu hivyo, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Rehema Nchimbi alisema vitabu hivyo vitatumika kuendeleza elimu katika mkoa huo na kuwakwamua wengi katika utumwa wa kifikra.

 “Udhamini huu wa Airtel utasaidia maendeleeo ya sekta ya elimu katika mkoa wetu wa Dodoma na kusaidia wanafunzi wengi waweze kuvutika katika usomaji wa vitabu mbalimbali kujikomboa na ujinga na umaskini ambao umekuwa ni  tatizo kubwa sio tu kwa Dodoma bali kwa nchi nzima”.

 Akizungumza kwa niaba ya kampuni ya Airtel kuchangia elimu nchini Meneja Mauzo wa Kanda Bw, Stephe Akyoo Alisema “Airtel inatoa vitabu hivi katika dhumuni la kuhakikisha kiwango cha elimu nchini kinainuka na kuleta ukombozi wa kiuchumi na kimaendeleo kwa jamii na nchi kiujumla”.

Nae Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Bihawana Dodoma Crispin Mtesigwa alisema “Tunashukuru Airtel kwa kutoa vitabu hivi kwa shule mbalimbali za sekondari hapa nchini na huo ni mchango dhahiri wa maendeleo kwa nchi nzima. Ni jukumu letu sisi walimu na wanafunzi kuhakikisha vitabu hivi vilivyotolewa na Airtel vinatumika kama ilivyokusudiwa”

Kupitia mradi huo wa shule yetu, mpaka sasa shule zaidi ya 1,000 zimeweza kunufaika na mradi huo kwa kujipatia vitabu vya kiada hasa kwenye masomo ya Fizikia, Hisabati, kemia na Biolojia. mradi huu wa Shule yetu unasambaza vitabu kwa shule za sekondari kuanzia kidato cha kwanza mpaka cha nne pamoja na vitabu vya  walimu kwa ajili ya kufundishia.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.