ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, May 31, 2013

PEPSI KUDHAMINI MEYA CUP MIAKA MITATU MFULULIZO

Mstahiki Meya wa jiji la Mwanza Stanslaus Mabula (kulia) akizungumza na vyombo vya habari juu ya udhamini wa mashindano ya Meya Cup 2013, katikati ni Meneja wa kampuni ya SBC  watengenezaji wa vinywaji vya Pepsi Nico Coetzer, na kushoto ni meneja mauzo Sharif Taki, wakati kutangaza rasmi udhamini wa Pepsi katika Meya Cup. 


Meneja wa kampuni ya SBC  watengenezaji wa vinywaji vya Pepsi Nico Coetzer akifafanua udhamini wa kampuni yake kwa mashindano ya Meya Cup 2013.


Meneja mauzo wa kampuni wa SBC Sharif Taki, akielezea jinsi zawadi zilivyonuia kubadilisha maisha ya wajasiliamali kupitia Meya Cup.


Sehemu ya waandishi wa habari walio hudhuria hafla hiyo ya Udhamini wa Pepsi kwa michuano ya Meya Cup.


Sehemu ya waandishi wa habari walio hudhuria hafla hiyo ya Udhamini wa Pepsi kwa michuano ya Meya Cup.
Zawadi ni kama ifuatavyo:-
A. Mshindi wa kwanza-
-   Bajaji yenye thamani ya SH. 4,000,000/=
-   Fedha taslimu                  SH  1,000,000/=
-   Kikombe cha Ushindi 
-   Medali kwa wachezaji wote

B. Mshindi wa pili
-   Fedha taslimu                  SH 1,500,000/=
-   Kikombe
-   Medali za wachezaji wote

C. Mshindi wa tatu
-   Fedha taslimu                  SH. 500,000/=
-   Kikombe
-   Medali kwa wachezaji wote

D. Mfungaji Bora -  Kikombe

E. Timu yenye Nidhamu- 
Aidha Meya wa jiji la Mwanza Stanslaus Mabula ametoa Shukurani kwa Mkurugenzi wa jiji la Mwanza na timu yake ya wataalamu wakishirikiana na My Way Entertainment katika kufanikisha kuratibu maandalizi ya mashindano ya Meya's Cup 2013.

Mwisho ametoa wito kwa wananchi na wanamichezo wote katika jiji la mwanza kushiriki pasipo kuchoka, wajue kwamba kuna fursa kubwa ya kushinda na hatimaye kujipatia zawadi kemkem na manufaa mengine kama yalivyoainishwa.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.