Katika ushindi huo Kocha wa Senegal Alilou Cisse ameweka historia kwani wakati timu hiyo inaifunga Ufaransa kwenye Finali za mwaka 2002 ndiye alikuwa nahodha.
Katika fainali hizo zilizopigwa nchini Korea ya Kusini na Japan, Ufaransa ndio walikuwa mabingwa watetezi baada ya kutwaa Kombe hilo mwaka 1998 kwa kuwafunga Brazil mabao 3-0.
Bao la kujifunga la mlinzi wa Poland na klabu ya S.P.A.L Thiago Cionek dakika ya 37, liliipa nguvu Senegal na kucheza kwa kujiamini hadi kipindi cha kwanza kinamalizika. Kipindi cha pili M'Baye Niang aliongeza bao la pili dakika ya 60, kabla ya Poland kufunga bao moja dakika ya 86 kupitia kwa Grzegorz Krychowiak.
Senegal sasa inashika nafasi ya pili kwenye Kundi H nyuma ya Japan zote zikiwa na alama 3. Poland na Colombia zinabanana mwisho baada ya wote kupoteza mechi zao za leo.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.