ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, January 25, 2018

JEMBEKA NA KILIMO.



VIJANA 6 wilayani #igunga wanaolima kwa kikundi huku wakicheza ngoma, wanapiga mzigo balaa. 

Baada ya mahojiano na #KAZINANGOMA niliwauliza, "kundi lenu linaitwaje....!!?" Wakasema ingawa wako kipindi kirefu katika kilimo wakilima mashamba ya wananchi kwa malipo ambayo kwayo wametengeneza ajira, lakini bado kundi lao hawajalipa jina....... Nikawaambia "Hamuwezi kwenda hivi hivi bila ya kuwa na jina la kundi watu watawatambuaje..!" Na ndipo wakanipa fursa niwachagulie jina.

Bila ajizi nikawabatiza kwa MAJI YA MOTO kundi lao nikalipa jina JEMBEKA NA KILIMO (ikiwa na maana 'fanya kilimo kama burudani ingawa inatupa pesa'. 

Wao wanafurahia sana kazi hii, kuanzia saa moja asubuhi hadi saa tisa wanauwezo wa kulima hekari 4, na kwa kila hekari moja gharama ya kulima au kupalilia ni shilingi elfu 15,000/= top... Haina mjadala. .

Hivyo wana uhakika wa kutoka na Tsh 45,000/= kwa siku. .

Jeh huoni kuwa hii itahamasisha vijana wengi kuwekeza kwenye ajira za kilimo kuliko kubanana na ajira za maofisini?..........
CC:- @jembenijembe @paulmakonda @eddievied @gijegije @mansourjumanne @deejaykflip @prince_nzwalla @johnjackson_jj @djmike_beatz @chrissthedj @djscopion @deejay_jacko @mustafakinkulah @johangasa4 @harith_jaha

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.