ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, May 3, 2013

MKURUGENZI WA JIJI LA MWANZA BW.KABWE AHAMISHIWA JIJI KUBWA NCHINI LA DAR ES SALAAM AMEWABEZA WANAOMZUSHIA NA KUMCHAFUA KWA KUTAFUTA UMAARUFU WA KISIASA.





Na Peter Fabian, MWANZA.                                02/05/2013
MKURUGENZI wa Jiji la Mwanza Bw.Wilson Mbonea Kabwe amehamishwa  Jiji la Dar es salaam taarifa zilizopatikana na kuthibitishwa naye pia na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza.

Mkurugenzi Mpya wa jiji la Dar es salaam.
Taarifa za kuhamishiwa Jiji la Dar es salaam ambalo ni kubwa kuliko yote nchini zimekuwa zikizungumzwa na baadhi ya watu wakiwemo wanasiasa na watumishi wa Jiji hilo lakini baadhi ya wanasiasa wamekuwa wakipotosha ukweli halisi wa uhamisho wa Bw.Kabwe ambapo baadhi yao wamekuwa wakidai amepelekwa Wizarani na wengine wakidai amehamishiwa Manispaa za Jijini Dar es salaam.

Akizungumza na Blog hii ofisini kwake Jijini Mwanza alisema kwamba taarifa za kwamba amehamishiwa Jiji kubwa kuliko yote nchini la Dar es salaam niza  ukweli na hata pale alipokuwa amekwenda kuhudhulia sherehe ya  maadhimisho ya Muungano na hata baada ya kurejea kwa  sasa Jijini hapa.

“Ni kweli naweza kusema kuwa nimepokea taarifa hizo za kuhamishiwa Jiji la Dar es salaam kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Jiji hilo na siyo Manispaa mojawapo kama baadhi ya watu na wanasiasa wanavyopotosha kwa umma wakidai nimeondolewa kwa matatizo ili kupisha uchunguzi.”alisema kuwa huo ni uzushi.

Aliongeza na kuthibitisha kwamba serikali imenihamishia Jiji hilo kwa kuona umhimu wangu na utendaji wa majukumu yangu ili kuendana na kasi ya ukuaji wa Jiji hilo na changamoto zinazolikabili kwa sasa katika sekta zote za kijamii,kiuchumi na kuwezesha kupatikana maendeleo” alieleza .

Bw.Kabwe ambaye alihamishiwa Jiji la Mwanza mwaka 2006 akitokea Jiji la Mbeya na kushirikiana na viongozi wa serikali za Wilaya ya Nyamagana na Ilemela wakati huo zikiunda Jiji la Mwanza kabla ya Augosti mwaka kugawanyika na kuundwa Manispaa ya Ilemela sasa.

 “Naondoka Jiji la Mwanza kwa heshima, kutokana na hivi karibuni taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG)kuonyesha na kulitaja Jiji la Mwanza kupata Hati Safi ya Mapato na Matumizi ya fedha za umma  kukidhi vigezo vya kupatiwa hati hiyo na kuyapita Majiji ya Dar es salaam ,Mbeya, Arusha, Tanga na baadhi ya Manispaa na Halmashauri za Wilaya hapa nchini”alisisitiza.

Aidha naliacha Jiji la Mwanza likiwa la Kwanza nchini kuchukua nafasi ya kwanza (Mshindi) wa Hati ya  Usafi na Mazingira kwa miaka saba mfululizo na pamoja na frusa tele za kuvutia wawekezaji katika sekta mbalimbali Jijini Mwanza ambayo hii ndiyo changamoto aliyoiacha na kutakiwa mrithi wake ajaye kuiendeleza kwa kusimamia kanuni na kuzitekeleza kikamilifu sheria za Mipango Miji zilizopo.

Taarifa ya zinazosambazwa na kutolewa kwa kupotoshwa na baadhi ya watu na chombo kimoja cha habari (Gazeti la kila siku nchini) Jijini Mwanza  kuwa Bw.Kabwe amihamishwa na serikali kupisha uchunguzi wa tuhuma za mgogoro wa viwanja (Ardhi) kati ya Jiji la Mwanza na Shirika la Hifadhi ya Mfuko wa  Jamiii (NSSF) katika eneo la Bugarika Wilayani Nyamagana kwa madai kuwa aliongoza Jiji hilo kujipatia fedha kiasi cha bilioni 1.6 ili kutoa viwanja 692 kwa NSSF lakini halikuweza kufanya hivyo.

“Ukweli na msingi wa madai hayo na Habari zilizoandikwa na Gazeti la Mwananchi la Mei mosi ni uzushi mkubwa na zisizo na ukweli hata chembe na iwapo kama kungekuwa na mgogoro na Shirika la NSSF nadhani taarifa zingetolewa uongozi wa NSSF na Wizara husika na serikali ya Mkoa wa Mwanza, suala la viwanja hivyo vinavyodaiwa ilikuwa ni makubaliano baina ya Jiji na NSSF na liliisha malizika na hakuna mgogoro  kama ambavyo baadhi ya wanasiasa wamekuwa wakilipotoshwa kwa wananchi.

“Kazi ya wanasiasa ni kusema kila jambo ambalo wanadhani ndiyo litawapatia umaarufu na mtaji wa kisiasa na njia ya kuungwa mkono na wafuasi wa vyama vyao ili kuweza kuwachagua na kurudi madarakani Mwaka 2015 lakini watambue kuwa sisi wataalamu ni watu wa kutekeleza taratibu,kanuni na sheria na si kuwatukuza wanasiasa na watu kwa masilahi ya yao binafsi na vyama vyao”alisisitiza.

Aliyekuwa Mkurugenzi wa jiji la Mwanza Wilson Kabwe (wa nne kutoka kushoto), Mstahiki Meya wa jiji la Mwanza Stanslaus Mabula (wa tatu kutoka kushoto) wakiwa na baadhi ya madiwani na wakuu wa idara wa jiji la Mwanza.
Sulala hili halipo kabisa ,NSSF walitaka viwanja kwenye mradi eneo la Bugarika tulivyopima lakini ikatokea wananchi wa maeneo yale kukubali kulipia garama ya viwanja hivyo na vikabaki viwanja vichache ambavyo havikukidhi mahitaji ya NSSF tukawaeleza na kukubaliana na hoja yetu tukasema kama wanahitaji basi tuwapatie eneo la kishili lililopo Katani Igoma na siyohivyo inavyozungumzwa.

Hata hivyo mgogoro huo tayari haupo na hata Kamati ya Bunge iliisha kutana na uongozi wa Jiji na NSSF na kusikiliza pande mbili hizo na kumalizika kutokana na Jiji hilo kuweka bayana huku likionekana kutoa upendeleo zaidi kwa NSSF kuwapatia maeneo ya kuwekeza ambapo ilisha toa eneo la Mwanza Tenesi Klabu lililopo Carpili point kwa ajili ya ujenzi wa Holeli ya hadhi ya nyota tano,eneo la kiliniki ya mbwa ambalo kwa sasa  kumejengwa jengo refu la la kitega uchumi la NSSF ikiwemo Hoteli ya JB Belamonte.

Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Bw.Baraka Konisaga alilieleza kwamba Jiji la Dar es salaam litakuwa limepata Mkurugenzi mchapa kazi na mtaalamu ambaye ni Mwanasheria atakaye zishughulikia changamoto mbalimbali zinazolikabili Jiji hilo na ndiyo maana serikali imemhamishia Mkurugenzi Kabwe kuhakikisha anashirikiana na wakurugenzi wa Manispaa na serikali kuu kuzitafutia ufumbuzi.

“Jiji la Dar es salaam linazo changamoto nyingi na zinazo hitaji ubunifu na utekelezaji wa sheria na Bw.Kabwe ni Mwanasheria mzuri na mtu anayejiamini, haya madai kuwa ameondolewa Mwanza kupisha uchunguzi ni uzushi lengo ni kumchafua lakini huwezi kuhamishwa ukapewa kituo kikubwa cha kazi kama Jiji la Dar es salaam kama unatuhumiwa kwa madai hayo yangekuwa na chembe ya ukweli basi angepelekwa Wizarani aidha akasimamishwa sio kuhamishiwa Jiji kubwa kuliko yote nchin”alisisitiza Mkuu huyo wa Wilaya.

Baadhi ya watu walimuelezea Bw.Kabwe kuwa ni Mkurugenzi makini ambaye anaifahamu kazi yake na amekuwa na msimamo ambao kwa namna moja umekuwa ni kikwazo cha baadhi ya wanasiasa na wafanyabiashara wanaorahisisha mambo na tangu kuwahamishiwa Jiji la Mwanza kumekuwa na mabadiliko makubwa katika sekta ya Uwekezaji,Miundombinu,Mipangomiji,Afya,Elimu na Usafirishaji.

Meya wa Jiji la Mwanza Bw.Stanislaus Mabula (CCM) alisema kwamba taarifa ya kuhamishwa kwa Mkurugenzi Kabwe anaisikia na kimsingi hajapata taarifa rasimi ya maandishi na kama itakuwa kweli basi Jiji la Mwanza ni la pili kwa ukubwa litasubilia Mkurugenzi atakayeteuliwa kushika nafasi hiyo nay eye na Baraza la Madiwani litafanya kazi na yeyote atakayepewa nafasi kwa vile Baraza na Watumishi ndiyo Jiji.

“Ni mapema kusema na kuzungumzia taarifa hiyo na ninachotambua wakurugenzi wote wanateuliwa kutokana na sifa zao za utendaji kazi hivyo sina mamlaka ya kuwajadili na Jiji la Mwanza halina mgogoro na NSSF kama inavyodaiwa na baadhi ya watu na wanasiasa ni kutaka kujitafutia umaarufu nap engine wao ndiyo wamekuwa sasa wasemaji wa Jiji na si Baraza la Madiwani na Mkurugenzi na timu yake”alisema Meya na kuongeza kuwa.

"Tutahakikisha Ilani ya Uchaguzi ya CCM inatekelezeka kwa kipindi cha miaka mitano tangu kupatiwa lidha ya kuunda serikali iliyopo madarakani kwa kuhakikisha huduma zinapatikana na kutolewa kwa wananchi katika sekta zote hapa Jijini pamoja na kuendelea kuboreshwa Nyanja za kiuchumi na kupatikana kwa maendeleo na wakati huu si wa kampeni ni wakati wa kutekeleza tuliyowaahidi wananchi."

Taarifa za ndani kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza zimeeleza kwamba uhamisho wa Bw.Kabwe ni wakawaida kwa watumishi wa serikali na hazina kwele yoyote na watu wanaojaribu kutoa taarifa zenye lengo ya upotoshaji kwa manufaa yao ama kujipatia umaarufu Fulani wa kisiasa na kijamii niza makusudi na kuhamishwa kwake pia ni kutokana na kukaa muda mrefu (miaka 8) eneo moja hatokea mara chache zaidi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.