ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, October 18, 2017

MBUNGE WA JIMBO LA KIBAHA MJINI SILVESTRY KOKA AKIPATIA MSAADA WA VYELEHANI KITUO CHA WALEMAVU CHA KWA MFIPA

Mbunge wa jimbo la Kibaha mjini Silvestry Koka akizungumza na wananchi katika moja ya mikutano yake.

 Katibu wa Mbunge wa jimbo la Kibaha Mjini Method Mselewa akizungumza na baadhi ya walemavu  hawapo pichani katika kituo hicho kabla ya kukabidhi rasmi vyelehani vine ambayo vitaweza kuwasaidia katika kujikwamua kiuchumi.(PICHA NA VICTOR MASANGU)

  Mwenyekiti  wa shirikisho la vyama vya watu wenye ulemavu  (SHIVYAWATA) Wilaya ya Kibaha mjini  Mohamed Mlanga ambaye ni mlemavu wa macho akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani mara baada ya kupokea vyelehani hivyo.

Afisa maendeleo ya jamii kata ya Kibaha Regina Mgovellah akizungumzia lengo la halmashauri ya Kibaha mji katika kuwasaidia walemavu wa aina mbali mbali.

 Baadhi ya walemavu pamoja na viongozi mbali mbali wa serikali na viongozi wa CCM kutoka jumuiya mbali mbali wakiwa katika picha ya pamoja nje ya jengo hilo la kituo cha walemavu mara baada ya kumalizika kwa halfa fupi za ugawaji wa vyelehani.

(PICHA ZOTE NA VICTOR MASANGU)
NA VICTOR MASANGU, KIBAHA  

KITUO cha watu wenye ulemavu wa aina mbali mbali kilichopo kwa Mfipa katika halmashauri ya Mji Kibaha Mkoani Pwani  kimepatiwa msaada wa vyelehani vinne kwa lengo la kuweza kuwasaidia katika kuendeshea shuguli zao  za ujasiriamali ili  kujikwamua kiuchumi, kupambana na wimbi la umasikini sambamba na kukabiliana na changamoto zinazowakabili hususan upatikaji wa mitaji na vitendea kazi.

Msaada huo ambao umetolewa na Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Silvestry Koka ikiwa ni utekelezaji wa ahadi yake aliyoitoa ya kuhakikisha anaweka mipango madhubuti ambayo itaweza kuwawezesha walemavu waweze kupata fursa ya kujiajiri wao wenyewe kupitia  shughuli za ujasiriamali na kuweza kupata kipato ambacho kitawasaidia kujikimu kimaisha.

Akikabidhi kwa niaba  msaada huo katika hafla fupi iliyofanyika katika ofisi za kituo hicho Katibu wa Mbunge huyo Method Mselewa  amesema kuwa msaada huo utakuwa ni mkombozi mkubwa kwani utaweza kuwasaidia kwa kiasi kikubwa  katika shughuli mbali mbali za ushonaji ambazo zitawapa fursa ya kujiingizia kipato na kujikwamua kiuchumi.

Katibu huyo alisema kuwa ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini inatambua uwepo wa kundi la watu wenye ulemavu hivyo wataendelea kushirikiana nao bega kwa bega katika kuwawezesha katika mambo mbali mbali ikiwemo kuwapatia mitaji pamoja na vitendea kazi ambavyo vitaweza kuwa ni mkombozi mkubwa katika suala zima la kuleba mabadilo ya kimaendeleo.
“Mimi nimekuja kwa niaba  ya Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini kwa hivyo ameniagiza kama katibu wake nije kutoa msaada huu wa vyelehani vine kwa kituo hiki cha walemavu  wa aina mbali mbali hivyo ninachokiomba viongozi wanaohusika kuhakikisha kuwa wanavitunza vifaa hivi ili viweze kuwasaidia na wengine wenye mahitaji katika siku za mbeleni na kuleta tija zaidi katika kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja pamoja na vikundi husika,”alisema Katibu huyo.

Naye Mwenyekiti  wa shirikisho la vyama vya watu wenye ulemavu  (SHIVYAWATA) Wilaya ya Kibaha mjini  Mohamed Mlanga ambaye ni mlemavu wa macho amempongeza Mbunge Koka kwa msaada huo wa vyelehani na kumwomba Rais wa awamu ya tano Dk.John Pombe Magufuli kuwasaidia kwa hali na mali  walemavu wote nchini  kuwawezesha katika kuwapatia  mitaji kwa ajili ya kufanyia shughuli za ujasiriamali.

Kwa upande wake  Afisa maendeleo ya jamii kata ya Kibaha Regina Mgovellah amesema kuwa lengo kubwa la ujenzi wa kituo hicho cha walemavu ni kwa ajili ya kuwakutanisha kwa pamoja na kuwapatia mafunzo mbali mbali ya ujasiriamali ili waweze kujikwamua kimaisha sambama na kuwasaidia katika kuwapatia   mahitaji mengine ya msingi.

HALMASHAURI ya mji Kibaha imeamua kuwajengea walemavu kituo hicho maalumu kwa ajili ya kuweza kuendeshea shughuli  zao mbali mbali  za ujasiriamali ambapo kwa sasa wameshaanzisha miradi mbali mbali ya ushonaji,kilimo  cha mboga mboga  ili kuweza kujikwamua kimaisha na kuleta mabadiliko chanya ya kimaendeleo ambapo kwa sasa kituo hicho kina jumla ya idadi ya walemavu 687.
     

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.