KOREAKaskazini imesema kuwa, katika
utekelezaji wa siasa zinazotajwa na Marekani za 'Uvumilivu wa Kimkakati'
hakuna utofauti yoyote baina ya Rais Donald Trump au mtangulizi wake
Barack Obama.
Gazeti la Rodong Sinmun la chama
tawala nchini Korea Kaskazini limeandika kuwa, Rais Trump anakusudia
kuendeleza njia ile ile ya makosa ya mtangulizi wake na kwamba kile
kinachoshuhudiwa hii leo hakina tofauti yoyote baina ya viongozi hao
wawili. Gazeti hilo limeongeza kuwa, siasa za Marekani zinazoitwa
'mkakati' au 'Uvumilivu wa Kimkakati' hazitakuwa na faida yoyote ghairi
ya uharibifu.
Kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un
Hii ni katika hali ambayo hivi karibuni Rex W. Tillerson, Waziri wa
Mambo ya Nje wa Marekani alinukuliwa akisema kuwa, siasa za uvumilivu wa
kimkakati zilizotekelezwa kwa miongo miwili iliyopita kwa ajili ya
kusimamisha mipango ya nyuklia ya Korea Kaskazini, sasa zimefikia
tamati. Wakati huo huo, Pyongyang imesema kuwa, hata hapo awali serikali
ya Barack Obama iliwahi kutangaza kufikia mwisho siasa hizo za
uvumilivu wa kimkakati na kwamba pamoja na hayo haikuweza kuchukua hatua
yoyote na badala yake iliendelea kufanya makosa ya muda mrefu.
Rex W. Tillerson, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, aliyedai kumalizika siasa za uvumilivu
Gazeti la Rodong Sinmun la chama tawala nchini Korea Kaskazini
limesisitiza kuwa, makosa ya siasa za Marekani hayatailetea faida nchi
hiyo, bali yatazidi kuisukuma Pyongyang kuweza kujiimarisha zaidi
kijeshi sambamba na kustawisha silaha zake za nyuklia kwa lengo la
kukabiliana na chokochoko hizo za Washington.
Ripoti hiyo imetolewa
katika hali ambayo duru za jeshi za Korea Kusini zimearifu kwamba, kuna
uwezekano mkubwa Korea Kaskazini ikafanya jaribio la sita silaha zake za
nyuklia katikati ya mwezi ujao wa Aprili, suala ambalo limeitia
tumbojoto serikali ya Seoul na waitifaki wake, yaani Marekani na Japan.
Chukua Mkwanja Wako Mapema Leo
-
HATIMAYE baada ya jana kushuhudia mechi kibao zikipigwa na matokeo mengine
yakiwa yakustaajibisha, leo hii ni zamu tena ya wababe wengine kibao
uwanja...
RAIS SAMIA AFTURISHA WATOTO KIKOMBO DODOMA
-
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe.
Mwanaidi Ali Khamis akigawa iftar kwa mmoja ya mtoto anayelelewa katka
Makao ...
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.