ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, October 1, 2016

SERIKALI IMEFANYA MABADILIKO YA VIONGOZI KWENYE USHIRIKA

NA ANNASTAZIA MAGINGA,Mwanza.

SERIKALI imefanya mabadiliko kwenye safu ya  uongozi wa tume ya maendeleo ya ushirika kwa kumteua Batholomew Haule kuwa kaimu mrajis wa tume hiyo ili kuboresha utendaji wa maendeleo ya Ushirika .

Akizungumza na waandishi wa habari jana Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi  Dk. Charles Tizeba amesema pamoja na kazi wanayoifanya tume hiyo, Serikali pia imedhamiria kukuza uchumi wa wananchi  kwa kutumia  dhana ya Ushirika.

“Serikali imefanya mabadiliko hayo na kutiliwa mkazo kufuatia hotuba ya waziri Mkuu wa alipokuwa akifungua mkutano wa nne wa bunge  la kumi na mbili  la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo waziri kuwa watakao bainika kuhusika na ubadhirifu wa mali za ushirika kuchukuliwa hatua hivyo sitegemei makosa hayo kujirudia”, Amesema Tizeba.

Viongozi wengine waliohamishiwa moshi katika chuo kikuu cha ushirika ni Dk. Audax Rutabazimbwa ( aliyekuwa kaimu mrajisi)  na Johnham Malewo  (aliyekuwa kaimu naibu mrajisi) huku wengine watumishi sita waandamizi wakitakiwa kuwasili kwa katibu mkuu Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi ili waweze kupangiwa vituo vya kazi.

Tizeba aliwataja  Viongozi hao wapya ambao wataenda kwa katibu kupangiwa kituo cha kazi kuwa ni pamoja na Peter Kasuga, Stephenson Ngonda, Bahati Lukiko, Moshi Mukama, Marwa Nyahende, Pamoja na Juma Makili.

“Katika kuimarisha huduma za  ushirika wafuatao watakaimu nafasi za warajisi wasaidizi katika mikoa ya Mtwara, Salmin Issa Lindi, Benjamini Magwala Njombe, Andrew Msafiri,  na Mara ni Richard Majalla na wale waliokua wanakamu nafasi za warasijisi wasaidizi watendelea kufanya kazi kwenye vituo walivyopo  sasa”, Alisema.

Hata hivyo mabadiliko hayo yamelenga katika kuboresha utendaji katika tasnia ya Ushirika huku akiwaagiza viongozi na maafisa wa ushirika kusimamia kikamilifu maendelao ya ushirika ili malengo ya kuanzisha yaweze kufikiwa ikiwa ni pamoja na kusimamia vyama utekelezaji wa sera na sheria ya ushirika

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment