ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, March 3, 2016

MADAKTARI WAWILI NA WAUGUZI WANNE WASIMAMISHWA KAZI KWA UZEMBE NA LUGHA CHAFU KUPELEKEA VIFO VYA WATOTO HOSPITALI YA WILAYA YA NYAMAGANA Pe

Na Peter Fabian, MWANZA.
MKUU wa Wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza, Baraka Konisaga, ameamuru Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza, Adam Mgoyi kuwasimamisha  kazi  madaktari wawili na wauguzi wanne katika Hospitali ya Wilaya ya Nyamagana iliyopo Kata ya Butimba kwa kushindwa kumuhudumia  mama mjamzito aliyefikishwa hospitalini hapo na kusababisha kujivungua watoto mapacha na badae kufariki.
Hatua hiyo inafuatia tukio la mgonjwa Suzana John (27) mkazi wa Kata ya Mkolani kufikishwa na ndugu zake katika Hospitali hiyo aliyekuwa mjamzito na kupokelewa na Dr Norin Magesa na Muuguzi Janet Foya waliokuwa zamu ya usiku siku ya March mosi mwaka huu majira ya saa 4:00 usiku na kushindwa kumuhudumia zaidi ya kutoa lugha isiyolizisha ikiwa ni pamoja na uzembe.
Awali DC Konisaga baada ya kufika Hospitalini hapo juzi majira ya saa 2:45 usiku wa March 2 mwaka huu na kukutana kwa dhalula na Mkurugenzi wa Jiji, Adamu Mgoyi, baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Nyamagana, Kaimu Mganga Mkuu Mkoa,Uongozi wa Hospitali na baadhi ya ndugu wa mgonjwa Suzana John aliyejifungua watoto mapacha waliokuwa hawajatimiza muda wao (Njiti) kisha vijanga hivyo kufariki baada ya kukosa huduma.
Katika kikao hicho cha dhalula kupokea maelezo ya pande mbili kutoka kwa wauguzi na familia ya mgonjwa Suzana na kupitia taarifa zilizokuwa zimeandikwa na Madaktari wawili waliomuona mgonjwa huyo ndipo DC Konisaga akamuagiza Mkurugenzi Mgoyi na Kaimu Mganga Mkuu kuwasimamisha kazi madaktari wawili na wauguzi wanne ili kupisha uchunguzi wa kitaalamu juu ya tukio hilo.
Konisaga aliwataja wanaotakiwa kusimamishwa kazi kuwani Dr Magesa na muuguzi Foya waliompokea mgonjwa wakiwa zamu ya usiku  wa March mosi mwaka huu na kushindwa kumpatia huduma zaidi ya kumtolea lugha chafu na uzembe huku wakishindwa kutoa maelezo wakati wa kukabidhi kwa majukumu kwa madaktari na wauguzi walioingia zamu ya asubuhi ya March 2 mwaka huu.
DC Konisaga pia alieleza kuwa pamoja na kuingia kwa madaktari na wauguzi wa zamu ya asubuhi ya March 2 bado hawakumjali na kumhudumia mgonjwa huyo huku baadhi wakitoa lugha zisizo za faraja kwa ndugu wa mgonjwa na hata alipozidiwa na kupewa taarifa na ndugu wa mgonjwa huyo hawakufika na mara kadhaa walikuwa wakifika na kutoka bila kumudumia pamoja na kumsikiliza akilalamika.
Aliwataja wengine wanaotakiwa kusimamishwa kazi mara moja ni Dr Emiliana Mvungi, wauguzi ni Maria Mkankule, Suzana Sindano na Bibiana Moshi ambao walikuwa zamu na kutomhudumia mgonjwa ambaye alijifungua katika mazingira hatarishi akiwa Hospitalini hapo bila kupatiwa huduma hali iliyopelekea kujifungua vichanga mapacha wakiwa hai lakini walifariki nusu saa baadaye kwa kutopewa huduma.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Magesa Mulongo alimwagiza Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dr Rweyendela Onesmo ambaye ni Mganga Mkuu Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa ya Sekou-Toure kupewa maelezo ya kina kutoka kwa Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo,Dr Nangi William na Mganga Mkuu wa Jiji, Dr John Andereaw juu ya kushindwa kuchukua hatua pamoja na kupewa taarifa hizo.
Mulongo pia alimuagiza Dr Onesmo kuunda tume ya uchunguzi itakayoshughulikia suala la tukio hilo na kisha kukamilisha kazi hiyo kwa siku moja na kumpatia taarifa ili hatua kali za maadili ya utumishi wa umma yachukue mkondo wake huku pia kuwezesha kusaidia jinsi ya kuboresha utendaji wa kitaalamu na kitabibu katika Hospitali hiyo ambayo kwa muda mrefu imekuwa ikilalamikiwa na wananchi kutokuwa na huduma nzuri kwa wagonjwa.
Akisimulia mkasa huo Dada wa mgonjwa Suzana aitwaye Estha John (35) mkazi wa Sengerema aliyekuwa akimhudumia alieleza kupata wakati mugumu ikiwemo kutolewa lugha za mauzi na wauguzi huku Daktari akishindwa kufika kwa wakati kuokoa maisha ya vichanga hivyo na kusababisha uzembe uliopelekea kupoteza maisha pamoja na kuzaliwa wakiwa na miezi sita sawa na wiki 24 kisha kufariki dunia.
Estha alisema kwamba vichanga hivyo viwili lilikuwa vya jinsia ya kike na kiume na tayari kulitokea mabishano makubwa baada ya kufariki kutakiwa kuchukua miili kwa ajili ya mazishi hali ambayo ilireta kutokuelewana na kusababisha ndugu wa familia ya mgonjwa ikiongozwa na mume wake Peter Michael (36) mfanyabishara mkazi wa Mkolani kutaka kupigana huku wananchi nao wakiunga mkono waliokuwa Hospitalini hapo.

Hali hiyo ilisababisha kuibuka kwa vurugu kubwa Hospitalini hapo na kupelekea viashilia vya uvunjifu wa amani na kupelekea DC Konisaga kufika hapo majira ya saa 2:45 hadi saa 5:45 usiku kufanya mazungumzo ya kina na familia ya mgonjwa na uongozi wa Jiji, Hospitali kabla ya kukubaliana kisha kutoa tamko la kusimamishwa kazi kwa madaktari na wauguzi hao kupisha uchunguzi wa kilichopelekea vifo vya watoto hao.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.