ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, May 30, 2025

SAMIA: TUSIGWAJIMANISED CHAMA CHETU, MAGWAJIMA TUYAACHE NJE.


Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amewataka wajumbe wa chama hicho kuhakikisha mchujo wa wagombea unafanyika kwa haki na weledi ili kulinda hadhi ya chama, akisisitiza kuwa ni muhimu kuepuka kuwapitisha watu wasiostahili.

Akihitimisha Mkutano Mkuu Maalum wa CCM Taifa leo Ijumaa, Mei 30, 2025, jijini Dodoma, Samia amesema chama kisiruhusu kuathiriwa na tabia za baadhi ya watu waliopoteza mwelekeo wa kisiasa.


“Tukitoa mwanya ndugu zangu, tukapitisha wanaotafuta tu, na mie niwemo, ndiyo tunapata wale wanaokwenda huko - chama kinakuwa Gwajimanised,” amesema Rais Samia na kuongeza, “Kwa vyovyote vile tusigwajimanised chama chetu, Magwajima tuyaache nje,”


Amesisitiza umuhimu wa kuwapima wagombea kwa sifa, maadili na uwezo wao, siyo kwa mapenzi binafsi, hofu au mahusiano ya karibu. Aidha, ameonya kuwa mtu ambaye hana uhusiano wa kweli na chama hawezi kusaidia, bali atakivuruga.


“Mcheza ngoma si yake lazima ataharibu... Ukicheza ngoma si yako utaharibu na utajulikana tu,” amesema kwa mafumbo ya kinadharia yaliyolenga kuhimiza uaminifu na ushirikiano wa kweli ndani ya chama.


KUHUSU KATIBA MPYA

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeahidi kuhuisha na kukamilisha mchakato wa Katiba mpya kabla ya mwaka 2030, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani yake ya uchaguzi ya mwaka 2025–2030.


Akizungumza jijini Dodoma leo katika Mkutano Mkuu Maalumu wa CCM, Mwenyekiti wa Kamati ya Ilani ya CCM, Profesa Kitila Mkumbo amesema hatua hiyo inalenga kudumisha demokrasia, utawala bora na mshikamano wa kitaifa.


Amesema CCM inaamini kuwa misingi ya utawala wa sheria, haki za binadamu na demokrasia ni msingi muhimu kwa maendeleo endelevu ya Taifa, na kwamba chama hicho kitaielekeza serikali kuweka mfumo wa kisheria wa kutekeleza falsafa ya uongozi ya 4R. 

Wednesday, May 28, 2025

NIC YATIKISA MIRADI MIKUBWA NCHINI TANZANIA SASA YABISHA HODI MV MWANZA

 NA ALBERT G.SENGO/MWANZA

Kutoka kwenye SGR inayopita kwa kasi, kuelekea kukamilika hadi kwenye daraja la JPM linalounganisha Kigongo na Busisi... na kutoka kwenye nguvu ya maji ya Bwawa la Nyerere hadi kwenye mawimbi ya Ziwa Victoria – NIC haichezi mbali! Sasa, Mfuko wa Bima wa Taifa (NIC) watingisha tena – safari hii wakitua kwa kishindo kwenye meli ya kisasa MV Mwanza! Hiki ni kielelezo cha namna NIC inavyobadilisha si tu taswira ya bima nchini, bali pia maendeleo ya taifa. Hebu tusikie, hatua kwa hatua, jinsi walivyofanikisha yote haya!.

Tuesday, May 27, 2025

'UDHAMINI WENYE TIJA! PAMBA JIJI FC YAVUNA FAIDA KUTOKA NIC'

 NA ALBERT G. SENGO/MWANZA

"Ushirikiano kati ya NIC Insurance na Pamba Jiji FC inayoshiriki Ligi Kuu ya Tanzania Bara, haukuwa tu juu ya udhamini wa jina au kuonekana kwa chapa yetu. Licha ya kupata nafasi kubwa ya kuonekana (visibility) na kueneza brand ya NIC kwa wapenzi wa soka, pia tumeshuhudia matokeo ya moja kwa moja ya kiuchumi. Kupitia uwekezaji wetu kwa timu ya Pamba, tumeweza kuzalisha faida inayokaribia mara tatu ya kile tulichowekeza — hii ni zaidi ya asilimia 300 ya mapato dhidi ya gharama" "Ushirikiano huu unaonyesha jinsi michezo inaweza kuwa jukwaa dhabiti la kibiashara na kijamii." Kauli ya Karim Mesharck Mkurugenzi wa Masoko na mawasiliano NIC Insurance

AZIZ KI KAZINI LEO OFISI MPYA WYDAD IKIMENYANA NA SEVILLA YA HISPANIA

 


NYOTA mpya wa Wydad Athletic, Stephane Aziz Ki aliyesajiliwa kutoka Yanga ya Tanzania mwishoni mwa wiki leo anawea kuwa sehemu kikosi cha timu yake mpya kitakachomenyana na Sevilla FC ya Hispania katika mechi ya kirafiki leo kuanzia Saa 4:00 usiku Uwanja wa Mohammed V mjini Casablanca.

Mechi hiyo ni sehemu ya maandalizi ya Wydad kwa ajili ya michuano ya Klabu Bingwa ya Dunia ya FIFA 2025 inayotarajiwa kufanyika nchini Marekani kuanzia Juni 15 hadi Julai 13.

Taarifa zaidi zinasema kwamba pamoja na mechi dhidi ya Sevilla ambao waliwasili jana Casablanca – Wydad pia watacheza na FC Porto ya Ureno Jumapili kukamilisha mbili za kirafiki kabla ya Klabu Bingwa ya Dunia.

Wydad imeachana na aliyekuwa Kocha wake, Rhulani Mokwena wa Afrika Kusini baada ya kumaliza nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya Morocco maarufu kama Botola Pro ikiwa na pointi 54, nyuma ya FAR Rabat iliyomaliza pointi 57 na mabingwa RSB Berkane waliomaliza na pointi 70 baada ya mechi 30 za msimu.

Wydad Athletic ambao sasa wapo chini ya Kocha wa nyumbani, Mohamed Amine Benhachem wamepangwa Kundi G katika Klabu Bingwa ya Dunia pamoja na Manchester City, wababe wa Italia Juventus, na Al Ain ya Falme za Kiarabu (UAE).
Mbali na Aziz Ki Wydad imeimarisha kikosi chake kuwa kuwasajili winga mkongwe, Nourredine Amrabat kutoka Hull City ya England na mshambuliaji Hamza Hanouri kutoka FUS Rabat.

MBOGGO ACHUKUA FOMU YA KUWANIA UBUNGE JIMBO LA TANGA KUPITIA ACT- WAZALENDO HUKU AKIHAIDI KUIREJESHA TANGA YA VIWANDA

 

 

Katibu wa Chama cha ACT -Wazalendo  Wa Jimbo la Tanga Mohamed Salim Ponda (kushoto)  akimkabidhi fomu ya kuomba kuteuliwa kuwa mgombea Ubunge Jimbo la Tanga mwanachama wao John Charles Mboggo  (katikati)  kulia ni Mwenyekiti wa Wazee Jimbo la Tanga (ACT Wazalendo) Zaharan Mohamed


Na Oscar Assenga, Tanga.

KADA wa Chama Cha ACT –Wazalendo Mkoani Tanga John Charles Mboggo amechukua fomu ya kuomba kuteuliwa kuwania Ubunge katika Jimbo la Tanga kupitia chama hicho huku akihaidi kuirejesha Tanga ya Viwanda ambayo ni ndoto kubwa ya wananchi wa mkoa huo.

Akizungumza leo na waandishi wa habari mara baada ya kuchukua fomu hiyo alisema lenbgo la kuchukua fomu ya kuwania Ubunge ni kutaka kuhakikisha anatoa mchango wake katika kurejesha viwanda vya Tanga ambavyo wananchi wamekuwa na kiu navyo.

Alisema kwamba kwa sababu viwanda ni ajira  na nguvu kazi ya Tanga wanaongelea kuna vijana asilimia 68 ya vijana wakitumika kwenye viwanda watakuwa na uchumi kwenye Jimbo hilo na Mkoa kwa Ujumla.

“Tanga tunaamini sisi ni watu tunaamini watu wa kuleta maendeleo na ndio maana tunawahamasisha wananchi wenye sifa za kupiga kura kujitokeza kwa wingi kushiriki kwenye zoezi la kura  kwa lengo la kuwachaguoa viongozi watakaowaongoza”Alisema



Aidha alisema kwamba wasione aibu kutokana na uwepo wa hila mbalimbali wanajua namna ya kubaliana nayo ili kuhakikisha hazijitokezi kwenye mchakato huo.

Awali akizungumza Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Jimbo la Tanga  Anasi Mohamed Rweymamu alisema kwamba wanaendelea kuwakaribisha wagombe na kura zao wa maoni ndani ya chama ndizo zitakazoamua nani anaweza kupeperusha tiketi ya chama hicho kwenye nafasi ya Ubunge.

Alisema kwamba ACT Wazalendo ndio chama pekee ambacho kinaweza kupeperusha vyema Bendera yake katika kuibuka na ushindi kwenye nafasi ya Ubunge Jimbo la Tanga na Tanzania kwa upekee.

Naye kwa upande Katibu wa ACT  WaaJimbo la Tanga Mohamed Salim Ponda alisema kwamba wapo kwenye maandalizi ya uchaguzi kama chama hicho Taifa kilipotangaza kwamba zoezi la kuchukua fomu kutoka Aprili 18 mwaka huu mpaka 31 mwezi Mei katika nafasi za Ubunge na Udiwani.

Alisema kwamba katika uchaguzi huo wamejipanga kwamba wagombea watakao wapitisha katika kinyang’anyiro cha Ubunge katika Jimbo hilo watakuwa imara kuhakikisha wanapeperusha vyema bendera hiyo.

KOKA KUCHELE AFUNGUKA MAZITO ALIVYOPAMBANA KUSAIDIA KUBORESHA NS KUINUA SEKTA YA ELIMU JIMBONI

 


NA VICTOR MASANGU, KIBAHA

Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Silvestry Koka katika kuunga mkono juhudi za Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kukuza  sekta ya elimu ameamu kutumia kiwango cha asilimia 85 za fedha za mfuko  wa maendeleo ya  Jimbo lake katika kuboresha na kuinua kiwango cha  ufaulu kwa wanafunzi ikiwa pamoja na  kuweka miondombinu rafiki kwa shule zilizopo pembezoni mwa mji.  

Koka ameyabainisha hayo wakati wa ziara  ya kikazi ambayo ameambatana na wajumbe wa kamati ya mfuko wa jimbo kwa  lengo la kuweza  kutembelea na kugagua miradi mbali mbali ya kimaendeleo ambayo baadhi yake  inatekelezwa kupitia fedha ambazo zinaotokana na mfuko wa Jimbo.
Katika ziara hiyo wajumbe wameweza kupata fursa ya kutembelea katika shule ya msingi Misugusugu kwa lengo la kuweza kugagua utendaji wa kazi ya mashine kwa kunakili nakala za karatasi  (Photocopy shine )  ambayo imegharimu kiasi cha shilingi milioni 4.5 pamoja na kutembelea mradi wa jengo la ofisi ya mtaa wa Miembesaba 'B'.

Aidha katika ziara hiyo Mbunge Koka na kamati hiyo wameweza kutembelea mradi wa ujenzi wa mradi wa kalavati mtaa wa mpakani kata ya Mkuza ambapo limeweza kukamilika na kuwa mkombozi mkubwa kwa kuwasaidia wananchi wa aeneo hilo kuweza kupita kwa urahisi hasa katika kioindi cha mvua.

"Ndugu zangu kwanza kabisa nipende kuchukua fursa hii kumpongeza kwa dhati Rais wetu wa awamu ya sita Dkt. kwa kuweza kutenga fedha nyingi katika Jimbo la Kibaha mjini ambazo zieweza kwenda kuwa ni mkombozi mkubwa katika kutekeleza miradi mbali mbali ya maendeleo na kutatua kero na changamoto za wananchi,"amebainisha Mbunge Koka
 
Kadhalika katika ziara hiyo ya wajumbe hao wamewweza kupata fursa ya  kukagagua mradi wa ujenzi wa maboma ya madarasa mawili katika shule ya msingi boko Timiza  ikiwemo sambamba na kutembelea utengenezaji wa vitanda vya wanafunzi wa shule ya sekondari ya wasichana ya Kibaha lengo ikiwa ni kuboresha sekta ya elimu.

Diwani wa Kata ya Misugusugu Upendo Ngonyani amemshukuru kwa dhati Rais wa awamu ya sita Dkt. samia Suluhu Hassan pamoja na Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Silvestry Koka kwa kuweza kupambana kwa hali na mali kutekeleza ilani ya chama kwa vitendo ikiwa sambamba na kuwasogezea huduma mbali mbali za kijamii wananchi na kupelekea kupunguza kwa kiais kikubwa changamoto ambazo zilikuwa zikiwakabili.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Kongowe Hamis Shomari hakusita kumpongeza kwa dhati Mbunge Koka kwa kuweza kuwa mstari wa mbele katika kuboresha sekta ya elimu kwa kutoa fedha za mfuko wa Jimbo ambazo zimeweza kwenda kusaidia kwa kiais kikubwa katika suala zima la kuboresha miundombinu  ya majengo ya madarasa na kuchangia madawati  na kufanya wanafunzi kuondokana na adha ya kukaa chini.

Ziara  ya wajumbe wa kamati ya  mfuko wa maendeleo ya Jimbo la Kibaha imeweza kufanya ziara hiyo ya kukagua miradi mbali mbali ya maendeleo katika kata ya Misugusugu, Kongowe, Kibaha, Tumbi, pamoja na  kata ya Mkuza katika sekta za elimu, miundombinu ya barabara, mradi wa ujenzi wa ofisi ya serikali  pamoja na huduma za kijamii.

Wednesday, May 21, 2025

AISHI MANULA ASAFIRI NA SIMBA SC ZANZIBAR MECHI NA BERKANE

 

KIPA Aishi Salum Manula amesafiri na kikosi cha Simba kwenda Zanzibar kwa ajili ya maandalizi ya mwisho ya mchezo wa marudiano wa Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya RSB Berkane ya Morocco Jumapili.


Katika mchezo huo utakaoanza Saa 10:00 jioni Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar, Simba inatakiwa kushinda 3-0 ili kutwaa taji hilo au ishinde 2-0 na bingwa apatikane kwa mikwaju ya penalti.


Aishi hakusafiri na timu katika mchezo wa kwanza Simba ikifungwa 2-0 Jumamosi iliyopita (Mei 17, 2025) Uwanja wa Manispaa ya Berkane mjini Berkane nchini Morocco.


Mabao ya RSB Berkane yalifungwa na kiungo Msenegal, Mamadou Lamine Camara dakika ya nane na mshambuliaji Oussama Lamlaoui la pili dakika ya 14.


Tayari CAF imesema bingwa wa Kombe la Shirikisho atapewa Kombe jipya kama ilivyo katika Ligi ya Mabingwa Afrika, ambayo yatazinduliwa kesho katika ofisi za wadhamini wakuu, TotalEnergies Jijini Johannesburg, Afrika Kusini – Hafla itakayoanza Saa 12:00 jioni na kuhudhuriwa na magwiji wa soka barani Afrika.

WANANCHI KITONGOJI CHA KWAKIBOSHA KATA YA MAPINGA BAGAMOYO WAIOMBA SERIKALI KUINGILIA KATI SAKATA LA KUBOMOLEWA NYUMA ZAO.

 HABARI NA VICTOR MASANGU, BAGAMOYO, PWANI

SAUTI NA ALBERT G.SENGO Wananchi zaidi ya 120 wa kitongoji cha Kwakibosha Kata ya Mapinga Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani wameiomba Serikali kuingilia kati sakata la kukithiri kwa wimbi la matapeli wa ardhi ambao wamekuwa wakiwanyanyasa na kuwaonea kwa kipindi cha muda mrefu ikiwemo kuwavunjia nyumba zao za makazi na kupelekea kukosa maeneo ya kuishi. Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakati wa mkutano maalmu wa hadhara wamesema kwamba kwa sasa wamekuwa wakiishi katika mazingira magumu kutokana na nyumba zao 12 kubomelewa na mmoja wa wanannchi anayejulikana kwa jina la Peter Junior na kuomba mamlaka zinazohusika achukuliwe hatua kali za kisheria ili iwe fundisho kwa wengine. Kwa upande wake Mwenyekiti wa kitongoji cha Kibosha Shaban Rashid akizungumzia kuhusiana na hatma ya wananchi juu ya mtu huyo anayedaiwa kuwasumbua kwa muda mrefu amebainisha kusikitishwa kwake na vitendo vinavyofanywa na mtuhumiwa huyo ambaye amekuwa akiwanyanysa wananchi kwa kuwavunjia nyumba zao.

KUPITIA MRADI WA FEMA AILEADERS WABUNGE WABUNIFU NA MAKUNDI MENGINE WAPIGWA MSASA AKILI MNEMBA

 

Na Mwandishi Wetu,Dar es Salaam


Kupitia Mradi wa FemAILeaders, Shirika la Women Political Leaders (WPL), GIZ Makao Makuu, GIZ Tanzania na Omuka imeandaa Mafunzo ya Akili Mnemba “Artificial Intelligence - AI” yaliyoanza Mei  19 hadi 20 mwaka 2025, Dar es Salaam yaliyolenga mambo mbalimbali ikiwemo ulinzi wa mtandao,ubunifu na matumizi ya AI.


Mafunzo haya yaliwaleta pamoja Wabunge, Wabunifu na Makundi mengine kwa lengo la kuangazia ubunifu na matumizi ya AI, ulinzi wa kimtandao, utatuzi wa changamoto za AI na uhitaji wa kisera.

Delegation ya Bunge iliongozwa na Mhe Salome Makamba na kujumisha Mhe Prof Joyce Ndalichako, Mhe Esther Matiko, Mhe Ng’wasi Kamani na Makatibu wa Kamati za Bunge, Adv Ganjatuni Kilemile na Pius Katabazi.

 

Tanzania imeendelea kuongoza barani Afrika kwa Kuimarisha Uelewa na Ushawishi wa Wabunge Wanawake ili wawe Vinara wa AI hivyo kuchangia kwa Tanzania kunufaika na fursa zinazotokana na Akili Mnemba - AI. Tanzania imechaguliwa kuwa Mfano wa Kuigwa barani Afrika katika eneo hili. 

 

Aidha, Mradi wa FemAILeaders umeweza kufanyika Tanzania kufuatia jitihada za Mhe Neema Lugangira (Mb) ambae pja ni Mwakilishi wa Afrika/Mjumbe Maalum wa Afrika wa Shirika la Women Political Leaders (WPL) hivyo ametumia nafasi hiyo kuileta fursa hii Tanzania.
 

BENKI YA CRDB KUIWEZESHA ZANZIBAR KUJENGA SHULE 23 ZA GHOROFA

 

Zanzibar. Tarehe 21 Mei 2025: Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi ameipongeza Benki ya CRDB kwa jitihada zake za kusaidia utekelezaji wa miradi ya maendeleo baada ya kusaini mkataba wa mkopo nafuu wa takriban Euro milioni 80 (shilingi bilioni 240).

Akizungumza kwenye hafla ya kutiliana saini mkopo huo kati ya Benki ya CRDB na Wizara ya Fedha na Mipango Zanzibar, Rais Dkt. Mwinyi amesema maendeleo ya taifa yanahitaji ushirikiano wa serikali na sekta binafsi na Benki ya CRDB imekuwa ikionyesha hilo kwa vitendo kwa kujitoa kwake kila inapohitajika kufanya hivyo.
“Mkopo wa Euro milioni 79.962 utatusaidia kujenga shule 23 za ghorofa mbili. Shule hizi zitajengwa Pemba na Unguja hivyo kusaidia kutatua uhaba wa vyumba vya madarasa kwa kiasi kikubwa. Lengo letu ni kuwaona vijana wetu wanasoma katika mazingira rafiki ya kukua kiumri na kielimu,” amesema Rais Dkt. Mwinyi.


Uboreshaji huu wa mazingira ya shule, Rais amesema ni muhimu ili kuwapata viongozi bora, madaktari, wahandisi, wahasibu, wanasheria na wasomi wengine mahiri hivyo ni lazima kuwekeza kwenye elimu.
“Kila mtu mwenye maono mazuri anatambua umuhimu wa elimu hivyo mkopo huu utakaoboresha miundombinu, umekuja kwa wakati sahihi sasa hivi. Nawapongeza Wizara ya Elimu kwa kulifanikisha hili kwani ilikuwa nikipita wananchi wanaomba shule ya ghorofa kila mahali mpaka kule Tumbatu. Sasa suala hilo limekamilika na fedha za ujenzi wake ndio hizi hapa,” amesema Rais Mwinyi.

Benki ya CRDB imetoa mkopo huo kwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ikishirikiana na Benki ya Deutsche ya nchini Hispania kwa malengo ya kufanikisha ujenzi wa shule hizo zitakazokuwa na madarasa ya kisasa, vyoo bora, bustani za kuvutia, ofisi nadhifu za utawala, maabara na maktaba za kisasa pamoja na viwanja safi vya michezo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Adulmajid Nsekela amesema kwa muda mrefu wamekuwa wadau muhimu wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayosimamiwa na Serikali zote yaani ile la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa lengo la kuboresha maisha ya wananchi wanaoishi mjini au vijijini.


“Kwa hatua tuliyofikia, kwa sasa pande zote yaani Benki ya CRDB, Benki ya Deutsche na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar tunakamilisha masharti ya awali ya mkopo kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa miradi kusudiwa. Ni matumaini yetu kuwa masharti haya ya awali yatakamilishwa kabla ya mwishoni mwa mwezi ujao hivyo kuwezesha kuanza haraka iwezekanavyo utekelezaji wa mradi huu,” amesema Nsekela.
Nsekela ameongeza kuwa mkopo huo unajumuisha Euro milioni 69.312 sawa na asilimia 85 utakaotolewa kwa ushirikiano wao na Benki ya Deutsche huku kiasi kilichobaki cha Euro milioni 10.65 sawa na asilimia 15 kitatolewa na Benki ya CRDB peke yake suala lililopata baraka zote za SMZ kupitia Wizara ya Fedha na Mipango.

Nsekela pia amempongeza Rais Dkt. Mwinyi kwa juhudi zake za kuimarisha uchumi wa Zanzibar ikiwamo uuzaji na uorodheshaji wa Hatifungani ya Sukuk iliyotolewa na SMZ mapema mwaka huu na kukusanya shilini bilioni 381 kwa ajili ya ujenzi wa miradi ya maendeleo kwa kufuata misingi ya dini ya Kiislamu.
Benki ya CRDB imekuwa mdau mkubwa wa maendeleo visiwani Zanzibar ikishiriki kufanikisha miradi yenye thamani ya shilingi bilioni 130. Kwa mkopo uliosainiwa, unaifanya Benki ya CRDB kufikisha jumla ya shilingi billion 375 ya uwezeshaji wa miradi inayosimamiwa na SMZ.





Monday, May 19, 2025

MADAKTARI BINGWA 47 WATIA NANGA MKOANI LINDI KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA

 

Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi, Bi. Zuwena Omary akizunguza wakati  kuwapokea rasmi madaktari bingwa 47 chini ya mpango wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, awamu ya tatu, kwa ajili ya kutoa huduma za kibingwa katika hospitali zote za wilaya ndani ya mkoa huo.
Baadhi ya Madaktari bingwa ambao wamewasili mkoani Lindi kwa ajili ya kutoa huduma za kibingwa kwa wananchi wote mkoani.

Na Fredy Mgunda, Lindi.

Serikali ya Mkoa wa Lindi imewapokea rasmi madaktari bingwa 47 chini ya mpango wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, awamu ya tatu, kwa ajili ya kutoa huduma za kibingwa katika hospitali zote za wilaya ndani ya mkoa huo.


Akizungumza wakati wa mapokezi hayo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi, Bi. Zuwena Omary, alisema kuwa ujio wa madaktari hao ni sehemu ya jitihada za serikali kusogeza huduma za afya karibu na wananchi, hasa wale walioko maeneo ya vijijini ambako awali walilazimika kusafiri mbali kupata huduma za kibingwa.


“Huduma hizi zitapatikana katika maeneo saba ndani ya mkoa kwa siku sita mfululizo kuanzia leo. Lengo ni kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma bora na kwa wakati,” alisema Bi. Omary.


Aliongeza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan imekuwa mstari wa mbele kuboresha sekta ya afya kwa kujenga miundombinu ya kisasa, kununua vifaa tiba vya kisasa, pamoja na kuongeza wataalamu mbalimbali wa afya nchini.


Kwa upande wake, Mratibu wa timu hiyo ya madaktari, Michael Mbele, alieleza kuwa madaktari hao wamejipanga kikamilifu kutoa huduma zote muhimu za afya kwa wananchi wote, bila ubaguzi, katika hospitali za wilaya walizopangiwa.


“Tumewakilishwa na wataalamu wa kada zote za afya, kuanzia magonjwa ya ndani, watoto, wanawake, upasuaji na hata huduma za kisaikolojia. Huduma zote hizi sasa zitapatikana katika hospitali za wilaya,” alisema Mbele.


Wananchi wa Mkoa wa Lindi waliopata fursa ya kuhudumiwa walieleza furaha na shukrani kwa serikali, hususan kwa Mheshimiwa Rais, kwa kuendelea kuboresha huduma za afya nchini, hatua ambayo wameitaja kama ya kipekee na ya kupongezwa.

Saturday, May 17, 2025

SERIKALI YATAKA TAMISA ISIMAMIE KWA UADILIFU SHUGHULI ZA SEKTA YA MADINI ILI KUWANUFAISHA WAZAWA

WhatsApp%20Image%202025-05-16%20at%201.12.46%20PM%20(1)

Mwenyekiti wa Kamati ya Mawasiliano na Masoko ya Chama cha Wasambazaji wa Huduma katika Sekta ya Madini Tanzania (TAMISA), Dkt. Sebastian Ndege akifafanua jambo wakati wa kongamano la TAMISA lililofanyika jijini Dar es Salaam leo Mei 16, 2025.

WhatsApp%20Image%202025-05-16%20at%201.12.44%20PM%20(2)
Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Eng. Yahya Samamba akizungumza jijini Dar es Salaam leo Mei 16, 2025 katika uzinduzi wa Kamati ya Masoko na Mawasiliano ya TAMISA.
WhatsApp%20Image%202025-05-16%20at%201.12.45%20PM
Katibu wa TAMISA, Dkt. Theresia Numbi akizungumza katika uzinduzi wa Kamati ya Masoko na Mawasiliano ya TAMISA lililofanyika jijini Dar es Salaam leo Mei 16, 2025.

SERIKALI  kupitia Wizara ya Madini imeitaka  Chama cha Wasambazaji wa Huduma katika Sekta ya Madini Tanzania (TAMISA) kusimamia kwa weledi na uadilifu shughuli zote za sekta ya madini nchini ili kuhakikisha rasilimali hizo zinawanufaisha Watanzania, hususan wazawa.

Hayo ameyasemaleo Mei 16, 2025,  Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Eng. Yahya Samamba wakati akizungumza katika uzinduzi wa Kamati ya Masoko na Mawasiliano ya TAMISA, alisema kuwa Tanzania kwa sasa ina zaidi ya masoko 40 na vituo zaidi ya 100 vya kuuzia madini, jambo linaloonesha mafanikio makubwa ya sekta hiyo.

Eng. Samamba alisisitiza kuwa mafanikio haya yatakuwa na tija endapo TAMISA itasimamia ipasavyo shughuli zinazofanywa na wazawa, sambamba na kutekeleza maono ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Waziri wa Madini ya kuhakikisha uchimbaji na usambazaji wa madini unaleta faida kwa taifa.

 “Tunapokusanya kodi pamoja na tozo zisizo za kikodi, hiyo ni hatua nzuri, lakini tukiweka nguvu zote katika ukusanyaji wa kodi bila kusimamia vizuri shughuli nzima ya sekta hii, manufaa halisi tutayaona baadaye tu baada ya Mwenyezi Mungu kutuwezesha kuwa na madini haya,” alisema Eng. Samamba.

Aidha, alieleza kuwa mabadiliko ya sheria na kanuni za sekta ya madini lazima yalenge kuwawezesha na kuwanufaisha wazawa, kwa kutoa ajira, mafunzo na kutumia teknolojia ya kisasa ili kuinua uwezo wa Watanzania kushiriki kikamilifu kwenye uchumi wa madini.

Amewataka TAMISA na wadau wake kuhakikisha wanazingatia masuala ya Local Content, ajira kwa vijana, pamoja na usimamizi wa teknolojia kwa maendeleo ya nchi.

 “Serikali imedhamiria kuhakikisha vijana wanapata ajira kupitia sekta hii, na hilo litawezekana tu ikiwa sheria zitasimamiwa ipasavyo,” aliongeza.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa TAMISA, Peter Kumalilwa, alisema wamekuwa wakipokea malalamiko kutoka kwa wazawa kuhusu kupewa kazi na kushindwa kuzifanya kwa viwango stahiki, hali inayochangia ukosefu wa uaminifu na migogoro katika sekta hiyo.

 “Tumejipanga kufanya tathmini ya kina ili kuongeza uaminifu na kupunguza migogoro,” alisema Kumalilwa.

Aliitaka serikali kutekeleza ahadi ya kuishirikisha TAMISA moja kwa moja kwenye zabuni za serikali, kama ilivyoahidiwa katika kikao cha Mei 1, 2025, jijini Dodoma.

 “Ushirikishwaji huu utasaidia wanachama wetu kujiandaa mapema na kuchukua hatua stahiki ili kushiriki kikamilifu katika zabuni hizo,” aliongeza.

Aidha, alitaja changamoto ya wageni kupewa kazi ambazo kisheria ni za wazawa, akiiomba serikali kuingilia kati na kuhakikisha ushirikiano kati ya wageni na wazawa unazingatia sheria za Local Content ili kulinda maslahi ya wazawa na kuleta tija kwa taifa.
WhatsApp%20Image%202025-05-16%20at%201.12.44%20PM
Katibu wa TAMISA, Dkt. Theresia Numbi, alieleza kuwa kuanzishwa kwa kamati maalum ya mawasiliano na masoko ni hatua ya kimkakati katika kusimamia utekelezaji wa shughuli mbalimbali katika sekta ya madini na sekta nyingine za kiuchumi.

Alisema TAMISA ni matokeo ya kikao kati ya Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, na wadau wa sekta ya madini kilichofanyika Januari 2024, ambapo ilielekezwa kuanzishwa kwa chombo kitakachowaunganisha watoa huduma na wamiliki wa leseni nchini.

 “Kuwepo kwa jukwaa la pamoja kutasaidia kuwashirikisha Watanzania katika sekta ya madini na kuhakikisha kipaumbele kinatolewa kwa bidhaa na huduma za wazawa,” alisema Dkt. Numbi.

Aliongeza kuwa usimamizi wa sheria na ushirikishwaji wa Watanzania katika sekta hiyo umechochea fursa nyingi ikiwemo ajira, mafunzo, utafiti, uhamishaji wa teknolojia na manunuzi ya bidhaa zinazozalishwa nchini.

“Niwataarifu Watanzania mliopo hapa kuwa fursa za kwenye migodi ni kwa ajili yetu sote Watanzania,” alisisitiza.
WhatsApp%20Image%202025-05-16%20at%201.12.43%20PM
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Sekta Binafsi, Raphael Maganga, alisema kuwa uzinduzi wa kamati hiyo una lengo la kuhakikisha sekta binafsi inakuwa na ushawishi mkubwa katika uchumi wa Tanzania kupitia madini.

“Tunataka sera zetu ziwezeshe sekta binafsi kufikia malengo. Lengo letu ni kuhakikisha sekta ya madini inazalisha mabilionea wa kutosha nchini,” alisema Maganga.

Mkutano huo umeonyesha dhamira ya serikali na wadau wa sekta ya madini kushirikiana kwa karibu ili kuhakikisha sekta hiyo inachangia kwa kiwango kikubwa katika maendeleo ya taifa kwa kuwezesha wazawa kushiriki kikamilifu.
WhatsApp%20Image%202025-05-16%20at%201.12.43%20PM%20(1)

WhatsApp%20Image%202025-05-16%20at%201.12.43%20PM%20(2)

WhatsApp%20Image%202025-05-16%20at%201.12.47%20PM

WhatsApp%20Image%202025-05-16%20at%201.12.47%20PM%20(1)
Matukio mbalimbali wakati wa kongamano la TAMISA lililofanyika leo Mei 16, 2025 jijini Dar es Salaam.
WhatsApp%20Image%202025-05-16%20at%201.12.44%20PM%20(1)
Picha ya pamoja.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa Kamati ya Masoko na Mawasiliano iliyozinduliwa leo, Dkt. Sebastian Ndege amesema, kutokana na Tanzania kuwa na aina mbalimbali za madini na kampuni za nje na ndani ya nchi kuwekeza, ni wakati wa watanzania kushiriki kikamilifu katika uchumi wa madini.

Amesema, wanafahamu kuwa wanayo haki ya kushiriki katika kutoa huduma lakini pia wanao wajibu wa kuhakikisha wanatoa huduma sahihi kwa wakati sahihi na weledi. “Sisi kama TAMISA kazi yetu itakuwa ni kusimamia wanachama wetu kuhakikisha kuwa wanafanya kazi kwa weledi na kuhakikisha kuwa tunafuata maadili ya utoaji huduma ili tuweze kuaminika na hili tutalisimamia kwa nguvu zetu zote,” amesema Dkt Ndege.