Thursday, October 17, 2024
Wednesday, October 16, 2024
RAIS RUTO KUMTEUWA MAKAMU WA RAIS MPYA IWAPO SENETI ITAIDHINISHA KUBANDULIWA KWA GACHAGUA
Rais William Ruto anatarajiwa kumteua naibu rais mpya iwapo Bunge la Seneti litaendelea na hatua ya kumtimua Rigathi Gachagua. Picha: Rigathi Gachagua/William Ruto.
Kuondolewa kwa Rigathi Gachagua ofisini kutakuwa ni tukio la kihistoria, kwani itakuwa mara ya kwanza kwa naibu rais aliye madarakani kukabiliwa na mashtaka ya kutokuwa na imani naye katika historia ya Kenya.
Tumaini la mwisho la Gachagua kuokoa wadhifa wake ni nini? Hatima ya Naibu Rais sasa iko mashakani huku Seneti ikitarajiwa kuanza kujadili mashtaka yake Jumatano, Oktoba 16, na uamuzi wa mwisho ukitarajiwa kufanywa Alhamisi jioni, Oktoba 17.
Matokeo ya mchakato wa kuondolewa kwake yanategemea ikiwa theluthi mbili ya maseneta watapiga kura kumuondoa ofisini.
Akizungumza na NTV, Wakili wa Mahakama Kuu Steve Ogolla alisema kuwa hatima ya Gachagua sasa iko mikononi mwa Seneti, kufuatia mahakama kukataa kusimamisha Seneti kuendelea na mjadala wa mashtaka ya kutokuwa na imani naye.
"Hii ilikuwa nafasi yake ya mwisho kusimamisha mchakato huu na hakufanikiwa. Ukweli ni kwamba hatima yake sasa iko mikononi mwa Seneti. Lakini, naamini pia amejiandaa kwa Seneti, tumeona amewasilisha majibu yake kwa hoja hiyo," Ogolla alisema.
Ni nini kitafuata ikiwa Gachagua ataondolewa na Seneti? Kuondolewa kwa Gachagua kutoka ofisini kunaweza kuacha pengo kubwa ndani ya serikali ya Kenya Kwanza, na kumlazimu mkuu wa nchi kuteua naibu rais mpya kufikia Ijumaa, Oktoba 18. "Kinachoweza kutokea baada ya kuondolewa ni kwamba rais anaweza kuteua mrithi wa Gachagua haraka.
Lakini kifungu cha 149 bado kinahitaji kuwa mgombea huyo apitishwe na Bunge la Kitaifa ndani ya muda wa siku 60, lakini wanaweza kufanya hivyo haraka," Ogolla aliongeza.
UANDIKISHAJI UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA WAFIKIA 45% NCHINI - WAZIRI MCHENGERWA
Amesema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari jana Oktoba 15, 2024 katika ukumbi wa Halmashauri ya jiji la Mwanza kwa lengo la kufikisha elimu na hamasa kwa Wananchi juu ya umuhimu wa kujiandikisha.
Mhe. Mchengerwa amewataka wananchi wenye sifa na wanaokidhi vigezo vya kugombea wajitokeze kuchukua fomu kuanzia Oktoba 26, 2024 mpaka Novemba 1, 2024 ili waweze kugombea nafasi mbalimbali za uongozi wa serikali za Mitaa na Vijiji.
Vilele Waziri Mchengerwa amewataka wasimamizi wa uchaguzi kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia Sheria, kanuni, miongozo pamoja na maelekezo ya usimamizi wa uchaguzi.
"Maelekezo yangu kwa wasimamizi wa uchaguzi kuzingatia kanuni viapo na kutekeleza majukumu kwa mujibu wa viapo vyao". Amesisitiza Mhe. Mchengerwa.
Aidha Mhe. Mchengerwa amewataka Viongozi wa vyama mbalimbali vya siasa kutoa elimu kwa wanachama wao juu ya kujiandikisha na kushiriki uchaguzi wa Serikali za mitaa.
Zoezi la kujiandikisha katika daftari la makazi limeanza rasmi Oktoba 11, 2024 mpaka Oktoba 20, 2024 ambapo kila Mwananchi mwenye sifa na vigezo anatakiwa kujiandikisha katika eneo analoishi ili aweze kushiriki zoezi la Uchaguzi wa Serikali za mitaa.
Tuesday, October 15, 2024
MAFIA BOXING PROMOTION WAUNGA MKONO KAMPENI YA RAIS DKT SAMIA SULUHU YA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA
Monday, October 14, 2024
RAIS SAMIA APOKEA MWENGE WA UHURU KWENYE KILELE CHA MAADHIMISHO MBIO ZA MWENGE WA UHURU MWANZA
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akihutubia viongozi mbalimbali pamoja na Wananchi wakati akihitimisha Kilele cha Mbio za Mwenge ambazo kitaifa zimefanyika Jijini Mwanza katika Uwanja wa CCM Kirumba tarehe 14 Oktoba, 2024. |
"Nimehitimisha Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru pamoja na Wiki ya Vijana hapa mkoani Mwanza. Ninawashukuru wote waliojitokeza kushiriki tukio hili la kihistoria ambapo Mbio za Mwenge wa Uhuru zimefikisha miaka 60."
"Pongezi kwa wote walioshiriki kuukimbiza kwa mwaka huu na kazi nzuri waliyofanya ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo"
"Nimepokea taarifa ya miradi yote iliyotembelewa katika mbio hizi ambayo inakwenda kunufaisha wananchi kwenye kila kona ya nchi yetu. Nimepokea mapendekezo na salamu za wananchi wa maeneo yote ulikopita Mwenge wa Uhuru, na kwa umakini na uharaka tutayafanyia kazi yale yote yaliyoainishwa kwa manufaa ya Taifa letu"
RAIS wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan leo Oktoba 14, 2024 amewaongoza Viongozi na Wananchi mbalimbali kwenye kilele cha mbio za Mwenge zilizoambatana na Wiki ya Vijana na Nyerere Day katika uwanja CCM Kirumba Jijini Mwanza.
Rais Samia akipokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Kiongozi wa mbio hizo Ndugu Godfrey Eliakim Mzava kwenye Kilele cha Maadhimisho Mbio za Mwenge wa Uhuru katika uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza. |
Matukio mbalimbali katika kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru katika uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza. |
TASAC YAFANYA MAZUNGUMZO NA KANALI MTAMBI KUIMARISHA USALAMA WA USAFIRI MAJINI
TPA kuanza usimamizi wa mwalo wa Kirumba wilayani Ilemela
Thursday, October 10, 2024
KAMATI YA BUNGE YAMPONGEZA RAIS DKT SAMIA SULUHU KWA KUCHOCHEA MAZINGIRA MAZURI YA UWEKEZAJI NCHINI
Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mariam Ditopile Mzuzuri akisisitiza jambo wakati wa ziara hiyo |
Na Oscar Assenga, MKINGA
KAMATI ya Kudumu ya Bunge Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo imempongeza
Rais Dkt Samia Suluhu kwa kazi kubwa anayoifanya kuchochea uwekezaji nchini
pamoja na kuweka mazingira mazuri kwa wafanyabiashara.
Pongezi hizo zilitolewa leo na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya
Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo Mariam Ditopile Mzuzuri wakati
wa ziara ya siku moja ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Uwekezaji na
Biashara ilipotembelea eneo Kituo cha Forodha za Tanzania na Kenya eneo la
Mkinga Mkoani Tanga.
Alisema kwamba mazingira hayo mazuri yamewekwa kwa
wafanyabiashara ambao tayari wapo kwenye biashara na viwanda ambavyo vinazalisha
bidhaa mbalimbal nchini
“Leo tumepata fursa ya kuja hapa kituo cha Forodha Horohoro kuona
namna kituo hicho cha pamoja baina ya Tanzania na Kenya sisi kama kamati tunawapongeza
kwani kituo hiki kazi yake kubwa kukusanya mapato kuhakikisha wafanyabishawa
kutoa Kenya wanaoleta bidhaa hawapitia njia za panya wanapitia hapo kutoa
ushuru na kodi stahiki pia bidhaa zinazotoka nchini na kwenda nchi jirani
zinatoa ushuru stahiki “Alisema
Alisema wanawapongeza kuongeza ukusanyaji wa mapato kwenye kituo
hicho kwa maana mwaka jana walipanga kukusanya jumla ya sh.Bilioni 77 lakini
walikusanya Bilioni 90 na kwa mwaka huu wa fedha wa 2024/2025 kota ya kwanza
Julai hadi Sept walipangiwa kukusanya Bilioni 25 lakini wamekusanya bilioni 34 wanaona
ni mafanikio.
“Sisi kama Kamati tunaiomba serukali na tutalisimamia lazima
waongeze ufanisi katika kituo hicho na kikubwa cha kwanza ambacho kimeelezwa ni
ununuzi wa scana kwa namna tulivyoona ukusanyaji wa mapato unaridhisha lazima
tupate scana na focklift kwa ajili ya kunyanyua mizigo tuweze kuongeza ufanisi
na mapat kupanda”Alisema
Aidha alisema kwamba inawezekana wanaotumia njia za panya ni
kutokana na kukaa muda mrefu wakati wa kupitisha mzigo na hivyo kuona shida
kupitishia hapa hivyo tunaiagiza Serikali ndani ya muda mfupi na wizara zote
husika na Waziri Dkt Jafo akae na Waziri wa Fedha ili kwa haraka scana na
focklift ziweze kupatikana na kuongeza ufanisi na kituo kifanye kazi ile
inayokusudiwa chini ya uongozi wa Rais Dkt Samia Suluhu na Serikali yake ya
wamu ya sita.
Awali akizungumza wakati wa ziara hiyo Waziri wa Viwanda na
Biashara Dkt.Suleiman Jafo amesema kwamba Serikali itahakikisha bidhaa zote
zinazopitishwa kwenye vituo vya Forodha katika mipaka ya Tanzania na nchi
jirani zinaendelea kuwa na viwango vinavyokidhi na kudhibitishwa na Shirika la
Viwango Tanzania (TBS) Wakala wa VipimoTanzania ( WMA) na Tume ya Ushindani (FCC).
Alisema kwamba lengo la kuhakikisha hilo ni kuwalinda watanzania
na walaji wa mwisho wa siku wafanye biashara na kamati imetoa maelekezo
kuhakikisha eneo hilo linakuwa na scana ambayo inaweza kuhakikisha mizigo
inakwenda kwa haraka sana.
“Hili la scana hapa tumelichukua na sio muda mrefu kupitia Wizara
ya fedha tutahakikisha Scana hiyo inapatikana pamoja nyenzo za kufanyia kazi
ikiwemo Focklift itakayokuwa ikinyanyua mizigo lakini niwashukuru Kamati ya
Bunge kwa kazi kubwa na niwaambie serikali itahakikisha mambo yote muhimu
yanatekelezwa lengo kubwa ni kuboresha utoaji huduma”Alisema Waziri Jafo.
Aidha alimshukuru R ais
Dkt Samia Suluhu kutokana na kazi kubwa inayoendelea katika maeneo mbalimbali
ya kimaendeleo na hata kamati ilivyotembelea eneo la Horohoro imeona kuna mafanikio
makubwa kwenye ongezeko la mapato.
“Lakini kuona jinsi gani Taasisi zinasaidia kuhakikisha biashara
eneo hilo mizigo isafirishwe vizuri baina ya nchi ya jirani kenya na bidhaa
zinazopita lazima zinakidhi viwango vilivyowekwa na kuthibitishwa na TBS na WMAna
FCC lengo kuwalinda watanzania na walaji mwisho”Alisema Waziri Dkt Jafo.
Akizungumzia suala la ubinafsishaji lililofanyika miaka ya nyuma
nchini alisema Serikali ilikuwa na nia njema kufanya ubinafsishaji lakini kwa
bahati mbaya malengo yalienda tofauti wengi waliopewa viwanda hawakufanya vizuri.
“Kama mnakumbuka hivi karibuni Rais Dkt Samia Suluhu alitoa
maelekezo kwamba viwanda hivyo vifufuliwe maeneo mbalimbali na nilikuja Tanga na
hivi karibuni tumekaa kikao na Hazina kubainisha viwanda vyote na kuona hatua
za kuchukua“Alisema
Waziri Dkt Jafo alisema mojawapo ya hatua hizo ni kuhakikisha viwanda
ambavyo vilikuwa havifanyi kazi waangalia namna bora ya kufanya kazi kwa
utaratibu wa kisheria na wapate wawekezaji wengine au waliokuwepo wahakikishe
ndani ya muda mfupi wanafanya uwekezaji ili viwanda viweze kufanya kazi na
kutengeneza ajira kwa watanzania.