ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, December 30, 2019

CHUO KIKUU INDIA KUFUNDISHA MADAKTARI MASUALA YA UCHAWI.

File photo of Ayurvedic doctors being trained by surgeons at Mumbai hospital in 2008Haki miliki ya picha
Chuo maarufu nchini India kimeanza kutoa kozi ya ngazi ya cheti kwa madaktari jinsi ya kutibu wagonjwa wanaopatwa mapepo au huyaona.
kozi hiyo ya miezi sita katika chuo kikuu cha Banaras Hindu (BHU) kwa mji wa kaskazini wa Varasanasi, kozi hiyo itaanza mwezi Januari.
Na pia kozi hiyo itakua inatolewa na kitengo cha afya ya akili na magonjwa yasiyo ya kawaida.
Msemaji wa chuo aliambia shirika la habari la India kuwa kitengo cha masomo ya uchawi kimeanzishwa.
''Kitengo hicho kinaitwa Bhoot Vidya na kunajihusisha na magonjwa yasiyo ya kawaida ama matatizo ya akili'' anasema Yamini Bhushan Tripathi mkuu wa kitengo hicho.
Aliongeza pia Chuo hiki ndo chuo cha kwanza kuanzisha kozi ya namna hiyo ambayo itafundisha masomo ya utabibu wa majini, mapepo na mizimu.
Matibabu yatatolewa kwa njia ya dawa za asili, miti shamba na masaji.
Kwa mujibu wa utafiti wa 2016 wa kitengo cha magonjwa ya akili (Nimhans) karibu asilimia 14 ya watu nchini India ni wagonjwa wa akili na mwaka 2017 shirika la afya duniani WHO inakadiria asilimia 20 ya Wahindi wanaweza kupatwa na msongo wa mawazo katika kipindi fulani katika maisha yao.
Lakini kuna chini ya wagonjwa 4,000 wa akili huwa wanaenda hospitali kupatiwa matibabu rasmi, kuna uelewa mdogo sana juu ya afya ya akili.
Lakini pia kutokana na unyanyapaa kusambaa sana , wagonjwa wachache ndio wanaenda hospitali wengi huenda kwa waganga wa kienyeji na kudhani kuwa watatibiwa matatizo yao ya akili.
Wengi wameonesha kulidhihaki tangazo hilo katika mitandao ya kijami, baadhi wameuliza serikali ya India je vipaumbele vyake vikwapi?
Taarifa ya kuwa chuo hiko cha serikali kitaanza kutoa kozi hiyo imepokelewa kwa maoni mbalimbali katika mitandao ya kijamii, wengi wakiuliza ni namna gani kozi hiyo itatolewa?

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.