ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, August 21, 2013

HATARI YA MAGONJWA AMBUKIZI KWA UCHAFU VYOO SHULE YA MSINGI NYANZA MKUU WA MKOA WA MWANZA ATOA SIKU MBILI USAFI KUFANYIKA LASIVYO KITANUKA!

Mkuu wa mkoa wa Mwanza Evarist Ndikiro akimnywesha dawa za kukinga na kuzuia maambukizi ya magonjwa ya Kichocho na Minyoo ya tumbo mmoja kati ya wanafunzi wa shule ya msingi Nyanza ya jijini Mwanza kama sehemu ya Uzinduzi wa Mpango wa Taifa wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele. 
Na ALBERT G. SENGO
Mwanza.

MKUU wa mkoa wa Mwanza Eng. Evarist Ndikilo ametoa agizo la siku mbili kwa uongozi wa shule ya msingi Nyanza kushughurikia suala la vyoo shuleni hapo kwani mazingira hayo sio rafiki kwa watoto.

Agizo hilo amelitoa leo wakati akizindua mpango wa Taifa wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele katika shule ya msingi Nyanza jijini Mwanza.

Ndikilo amesema kuwa mazingira ya huduma ya vyoo kwa watoto wa shule hiyo hayaridhishi na ni hatarishi kwa afya za wanafunzi wa shule hiyo kwani yanaweza kusababisha mlipuko wa magonjwa ya kuambukiza yanayoambatana na uchafu  hivyo amewapa siku mbili wakuu wa shule hiyo kulitatua suala hilo.

“Kabla sijafika hapa niliwatuma vijana wangu kuja kuangalia kwanza hali ya mazingira ya shule ikoje ambayo imepewa kipaumbele cha uzinduzi kwa niaba ya shule zote Mkoani hapa na ndipo wakanileteta jibu kuwa shule ile ina tatizo la choo kwa wavulana hivyo naawagiza ndani ya siku mbili watoto wapate pakujisaidia.”alisema Ndikilo.

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya utafiti wa Magonjwa ya binadamu (NIMR) Dr. Mwele Malecela akizungumza na waalimu, wanafunzi na wageni waliohudhuria Uzinduzi wa Mpango wa Taifa wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele uliofanyika kimkoa shule ya msingi Nyanza.
Aidha kwa mujibu wa Takwimu zilizotolewa  na Mkurugenzi wa mpango wa taifa wa utafiti wa magonjwa ya binadamu (NIMR) Dr.Mwela Malecela zinaonyesha kuwa wakazi wa mkoa wa mwanza wameathirika na ugonjwa wa kichocho na minyoo ya tumbo kwa 80% huku taifa ikiwa ni 12.7%.

Amesema kuwa ni bora magonjwa hayo kutibiwa  ili kuhakikisha watoto wanakuwa na Afya njema ili wawe na uwezo wa kuelewa  na kuleta maendeleo ya kimapinduzi katika Elimu.

Dr. Mwela amewaomba wazazi kwa kushirikiana na walimu wa shule za mkoani hapa kuhakikisha wanafunzi wanakunywa dawa za minyoo na kichocho ili wawe na Afya nzuri na bora.

Mratibu kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa jamii kupitia Mpango wa Taifa wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Dkt. Upendo Mwingira akitoa taarifa fupi ya shughuli hiyo ya kitaifa.
Magonjwa ambayo yalikuwa hayapewi kipaumbele ni Magonjwa ambayo yapo ndani ya jamii, hasa jamii maskini lakini hayapewi umuhimu kulingana na athari yake katika jamii.

Magonjwa ya Matende na Ngirimaji, minyoo ya tumbo, Kichocho, Trakoma na Usubi ni miongoni mwa magonjwa yanayoathiri jamii na kudhoofisha.

Inakadiriwa kuwa watu bilioni moja duniani kote tayari wameathirika. Zaidi ya watu bilioni mbili wako hatarini kupata maambukizi ya Magonjwa hayo.

Nchini Tanzania tafiti mbalimbali  zinaonyesha kuwa maambulkizi ya magonjwa haya hupatikana karibu maeneo mengi.

Kabla ya ugawaji dawa za Minyoo na Kichocho kwa watoto wa shule ya msingi Nyanza, wanafunzi hao walipewa chakula.

Wanafunzi wa Shule ya msingi Nyanza wakigawiwa chakula.

Chakula Time.
Huduma hii ua dwa za kinga tiba inatolewa bila malipo yoyote kwa kila mtoto kupitia dawa za Praziquantel na Albendazole ambazo zimethibitishwa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamiii kuwa ni salama, hazina madhara kwa Afya ya binadamu zinapomezwa kwa kufuata maelekezo yanayotolewa na wahudumu wa afya na walimu waliopatiwa mafunzo rasmi.
Wanafunzi wa darasa la saba kutoka kushoto ni Hamisi Omar na Mariam Lawrance wakipata chakula na wanafunzi wenzao ndani ya chumba cha darasa kabla ya kupatiwa dawa za Mpango wa Wizara ya Afya kudhibiti magonjwa yasiyopewa kipaumbele. 

Chakula kwanza.

Safu ya waandishi wa Habari kutoka kushoto ni Mashaka Bartazar wa gazeti la Majira na Jambo Leo, Albert G. Sengo wa Clouds Fm, Hanry Kavirondo wa Channel Ten na kulia ni Mwandishi wa Sahara Media

Kila mwanafunzi aliagizwa kuja na sahani toka nyumbani hivyo mara baada ya matumizi waliziosha kupitia bomba la shule.

Pipa la taka katika shule ya msingi Nyanza kwa hisani ya Wizara ya Afya.

Unyweshaji dawa unaenda sambamba na kujua uzito na kimo cha mtoto.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza akiendelea kusimamia zoezi la ugawaji dawa.

Kuna mada imewagusa wanafunzi hawa....

Njia ya kujikinga na Magonjwa ya Kichocho, Minyoo ya tumbo, Trakoma, na mengineyo yasiyopewa kipaumbele ni:-
-Kutumia dawa za kutibu na kudhibiti magonjwa ambazo hutolewa kila mwaka kwa jamii iliyoathirika.
-Kuzingatia usafi wa uso na mwili kwa ujumla.
-Kuzingatia usafi wa mazingira kwa ujumla
-Kutokuoga/Kutokuogelea/Kutokutembea kwenye maji yasiyo safi na yaliyotuama kama vile mabwawa na mifereji.
-Kujikinga na kuumwa na inzi, mbung'o, mbu na wadudu wengine wasambazao maambukizi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.