
Huyo anakuwa mchezaji mpya wa tatu Yanga kuelekea msimu ujao – baada ya kiungo raia wa Guinea, Balla Mousa Conte kutoka Sfaxien ya Tunisia na winga mzawa, Offen Francis Chikola kutoka Tabora United.
Casemiro ni mchezaji ambaye amekipambanua vyema kipaji chake ndani ya misimu michache ya kucheza soka ya Zanzibar kiasi cha kuwa tegemeo kwenye klabu yake na timu ya taifa ya visiwani humo.
Mshindi huyo wa Tuzo Mwanasoka Bora kijana msimu wa 2024-25 katika tuzo za Farafa Zanzibar – aliiwezesha Mlandege kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya PBZ Zanzibar na kuiwezesha pia Zanzibar Heroes kutwa Kombe la Mapinduzi Januari mwaka huu.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment