
Bao pekee la Twiga Stars lililoizamisha Harambee Starlets limefungwa na kiungo mshambuliaji wa Al-Nassr ya Saudi Arabia, Clara Cleitus Luvanga dakika ya 49.
Mchezo mwingine uliotangulia jioni ya leo Sudan Kusini iliichapa Burundi mabao 3-1 hapo hapo Azam Complex.

Harambee Starlets inamaliza na pointi tisa katika nafasi ya pili baada ya kupoteza mchezo huo wa kwanza kufuatia kushinda mechi tatu za awali, ikifuatiwa na Uganda, Burundi na Sudan Kusini ambazo kila moja imemaliza na pointi tatu.

Naye kiungo Diana Lucas Msewa wa Trabzonspor ya Uturuki, amechaguliwa kuwa Mchezaji Bora wa michuano hiyo huku Naijat Idirssa wa JKT Queens akichaguliwa Kipa wa CECAFA Women’s 2025.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment