ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, February 18, 2011

HIZI BANGI...

Kamanda Simon Sirro -Kutokana na juhudi za wananchi kushiriki kulisaidia jeshi la polisi kufichua waalifu nalo jeshi la polisi kuongeza nguvu katika misako yake kupitia oparesheni mbalimbali katika kipindi cha mwaka 2010 – 2011 mkoani mwanza Jeshi hilo limefanikiwa kukamata madawa ya kulevya aina ya bangi kiasi cha kilo elfu moja mia tano sabini na tano na gramu 4.96.

Hayo yamebainishwa leo na Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa mwanza Simon Sirro wakati alipozungumza na waandishi wa habari mbele ya ofisi zake huku akionyesha baadhi ya vidhibitisho hivyo vya madawa mbalimbali ya kulevya yaliyokamatwa na jeshi lake.

Hili begi lilifungwa kama la msafiri ambalo unaweza dhani kuwa lina nguo lakini humo ndani liliku na robota la bangi iliyoshindiliwa kiuhakika.

Misokoyo na mitenba ya bangi iliyonaswa.
Madawa mengine yaliyokamatwa ni pamoja na mirungi kilo 3,769.106, Gongo lita elfu 10,638, na Noti bandia zenye thamani ya shilingi milioni sita laki saba tisini na tano elfu.

Kutoka TBC1 Richard Leo akiripoti....Kupitia misako mbalimbali kwa mwaka 2010 hilo limefanikiwa kukamata gramu mia mbili na kumi za madawa ya kulevya aina ya Cocaine na kiasi cha gramu mia sita hamsini na tatu za madawa ya kulevya aina ya Heroine.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.